Kusulubiwa pamoja na kristo

Yesu alisulubiwa kimwili msalabani Kalivari. Ingawa hakutenda dhambi yoyote, alijiweka katika adhabu ya dhambi, ambayo ilikuwa kifo, hivyo angeweza kulipa madeni yetu na kutusamehe dhambi zetu ikiwa tunatamani kumwamini na kumfuata. Mtume Paulo aliandika “Nimesulubiwa pamoja na kristo….” Wagalatia 2:20. paulo hakusulubiwa katika msalaba wa kimwili. Alitumia msemo huu kama ishara kuelezea kwamba dhambi zetu lazima “zisulubiwe” lazima iwe “msalabani”, lazima zife na hivyo zisiweze kuongoza matendo yetu tena. Mtu anayeishi “maisha yaliyosulubiwa” ni mtu ambaye haruhusu dhambi iyatawale matendo yake kamwe, huishinda dhambi.