Neno la msalaba

“Neno la msalaba” au “ujumbe wa msalaba” ni injili yenye nguvu ya agano jipya ambayo inahubiri uhuru kutoka katika dhambi kwa kujitwika msalaba na kumfuata Yesu kila siku, baada ya kupokea msamaha wa dhambi kupitia kifo cha Yesu msalabani Kalivari. Kujitwika mslaba wako haimaanishi kubeba msalaba wa kimwili kama ule wa kalivari, bali inamanisha kukataa mawazo ya dhambi na tamaa zinazokuja katika akili yako, hivyo “unazisulubisha” kwa hali hiyo zinakua hazina nguvu yoyote ya kutuongoza. (1Wakorintho 1:18; Luka 9:23)