Kwa nini hatufurahii kila wakati? Kwa nini ni rahisi sana kuwa na wasiwasi na kujawa na machafuko? Kwa nini inachukua muda mrefu sana kufikia imani hiyo ya uhakika na yenye nguvu ambayo inazungumziwa katika Waebrania 10:22?
Je, hii si imani ya uhakika na yenye nguvu ambayo inatupa furaha na amani ambayo kila mtu anatafuta?
Machafuko yanaweza kuwa matokeo ya kufanya madai, kutaka kupendwa, au kuendelea kutaka kitu katika ulimwengu huu. Tunaweza kuwa na visingizio vingi na sababu za wasiwasi wetu na machafuko, kama vile tunavyowajali wengine n.k.
Ninapokuwa na utulivu, ninahitaji kupata kitu ndani yangu ambacho husababisha machafuko haya. Yesu pia alikuwa na vita ya kupigana, kama tunavyosoma katika Yohana 12:27: "Sasa roho yangu imefadhaika; nami nisemeje? Baba, uniokoe katika saa hii? Lakini ni kwa ajili ya hayo nilivyoifikia saa hii .Kisha akaomba kwamba jina la Baba litukuzwe. (Yohana 12:28))
Ikiwa tuko macho katika hali zetu kama Yesu alivyokuwa katika hali zake, tutakuwa na furaha ile ile ambayo Yesu alikuwa nayo na kwamba tunaposoma Waebrania 1: 9. Tunaona hapo kwamba msingi wa furaha hii kamilifu ni kupenda haki na kuchukia maasi - sio maasi kwa wengine, bali maasi ndani yetu wenyewe!
Tuna faraja hii yenye nguvu katika Waebrania 6: 11-12 "Nasi twataka sana kila mmoja wenu aidhihirishe bidii ile ile, kwa utimilifu wa matumaini hata mwisho; ili msiwe wavivu, bali mkawe wafuasi wa hao wazirithio ahadi kwa imani na uvumilivu.."
Mungu atupe neema ili tuweze kufahamu sababu ya machafuko ndani yetu wenyewe, na kuyashinda kikamilifu, kama vile Yesu alivyofanya. Kisha jina la Mungu linaweza kutukuzwa, na tuna furaha, amani, na pumziko katika hali zetu zote. Hii ni furaha kamili.