Nawezaje kujua Biblia ni kweli?

Nawezaje kujua Biblia ni kweli?

Nimesoma Biblia na kujifunza kutoka kwake Maisha yangu yote, lakini nawezaje kujua kwa kweli kwamba Biblia ni kweli kabisa?

6/3/20173 dk

Na Ukristo wa Utendaji

Nawezaje kujua Biblia ni kweli?

Umewahi kujiuliza swali “Nawezaje kujua Biblia ni kweli?” Ni swali kubwa. Najuaje hasa kwa kweli?

Nikitazama mtandaoni, naweza kupata majibu tofauti tofauti. Ukweli wa kihistoria na kisayansi, unabii uliotimia n.k. lakini nawezaje kujua kwamba Biblia inanihusu mimi moja kwa moja, katika Maisha yangu, katika siku hii na wakati tunaouishi?

Biblia imekuwa msingi wa Maisha yangu tangu nikiwa mdogo. Nakumbuka nikikaa na mama na kaka na dada zangu anatusomea hadithi za Biblia kabla ya kulala. Hadithi zilikua hai kwangu. Mashujaa wa Imani wakifanya mambo makubwa kupitia kwa Mungu. Yesu na mitume wakitenda miujiza. Hadithi hizi hazijaondoka akilini mwangu.

Zaidi ya kitabu cha hadithi

Kadri nilivyokuwa nakua nilianza kuelewa kwamba Biblia haikuwa kitabu cha hadithi tu. Nilijifunza kwamba hadithi na mafundishlo ya Biblia bado yanatumika leo. Hunionesha njia nayopaswa kuipitia katika Maisha yangu. Maisha ambayo Yesu na wanafunzi wake waliyaishi yamekuwa mfano wa namna ya kuishi katika Maisha yangu.

Nilimuuliza rafiki yangu kama angeweza kuniambia kidogo Zaidi kuhusu namna tunavyoweza kuwa na uhakika na inatumika hata katika wakati huu. Rafiki ni mzee, na ninajua kwamba ana hekima na uzoefu. Alisema yafuatayo: “Tunajua kwamba Biblia ni kweli na ni neno la Mungu, kwa sababu tunapofanya inachotuelekeza, matokeo yake ni kama Biblia inavyotuambia. Kwa mfano ninapotoa nakuwa mwenye furaha. Nikinyenyekea napokea neema. Ninapomwomba Mungu, hunisikia na kunijibu, n.k.” (2Wakorintho 9:6-7; Yakobo 4:6; Yeremia 29:12-14)

Jibu lake lina maana kwangu. Nimepitia haya mimi mwenyewe. Huanza na kuamini kwamba kile kilichoandikwa kwenye Biblia ni kweli na ninapofanya kilichoandikwa pale ninaanza kupata uzoefu kwamba sheria zilizoandikwa katika Biblia zinaweza kubadili Maisha yangu, na ndipo Imani yangu inapokuwa imara Zaidi.

Kuamini kumeathiri vipi Maisha yangu?

Ninapokumbuka Maisha yangu, naweza kuona hilo kwa miaka mingi nimekua mtiifu kwa neno la Mungu, Maisha yangu yamebadilika kweli. Ninajua kwamba bado nina safari ndefu kabla ya kumaliza kazi ambayo Mungu anataka kufaya maishani mwangu, lakini tayari ninaweza kuona kwamba mabadiliko tayari yamefanyika ndani yangu.

Kwa mfano, kwa asili ningeogopa juu ya kila jambo – mambo yajayo, mambo yaliyopita, familia yangu, kazi yangu n.k. lakini katika Wafilipi 4:6-7) inasema, “Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, Pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu. Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.”

Hakika nimefanya yale yaliyoandikwa katika ayah ii. Nimemwomba Mungu, ninmepambana dhidi ya hofu ambayo nimejaribiwa nayo kirahisi. Na taratibu lakini kwa uhakika nimegundua kwamba amani ya Mungu inakuja moyoni mwangu na akilini mwangu. Ninajifunza kumwamini na kutojali chochote, na ninapitia pumziko lilioahidiwa na amani inayotokana na hayo. Ninaona kwamba neno la Mungu ni kweli!

Muujiza mkuu kuliko yote

Kwa hiyo, ninapofikiria juu ya mashujaa wa imani ambao nilikuwa nikiwasikia, kama vile Daudi na Yesu na mitume, na miujiza iliyotokea, ninajua kwamba ninaweza kuwa mmoja wa hadithi hizo. Si kwamba ninaua majitu au ninageuza maji kuwa divai. Lakini ninabadilishwa kwa sababu ninaamini na kutii yale yaliyoandikwa katika Neno la Mungu. Huo ndio muujiza mkuu kuliko yote, na haungeweza kufanywa bila Neno la Mungu.

Ikiwa unauliza swali, “Nitajuaje kama Biblia ni ya kweli?” Nina jibu kwako. Jaribu kuishi maisha ambayo Biblia inatufundisha. Uwe mtiifu kwa yale ambayo Biblia inasema. Ndipo utaona kwamba Biblia ni kweli.

Chapisho hili linapatikana katika

Makala hii inatokana na Makala ya Ann Steiner awali ilichapishwa katika https://activechristianity.org/ imechukuliwa na kupewa ruhusa kwenye tovuti hii.