Ninampendaje Mungu?

Ninampendaje Mungu?

Nitajuaje kama Mungu ananipenda kweli? Ninawezaje kuonyesha upendo wangu kwake?

17/9/20254 dk

Na Ukristo wa Utendaji

Ninampendaje Mungu?

Wakati mwingine tunaweza kujiuliza ikiwa Mungu anatupenda kweli. Je, ninahitaji kufanya chochote ili kustahili upendo Wake? Ikiwa nimetenda dhambi, je, Mungu bado ananipenda? Ninawezaje kuonyesha upendo wangu ?

Mungu anatupenda bila kujali tumefanya nini. Yeye anapendezwa na sisi, Yeye anatuelewa, anajua yote kuhusu udhaifu wetu, na anajua juu ya nguvu zetu, Yeye alituumba jinsi tulivyo, na Yeye anataka mambo yaende vizuri kwa ajili yetu.

Tunamfikiria Mungu kama Baba, na inaweza kuwa rahisi kufikiri kwamba Yeye ni baba ambaye anataka tu kutuadhibu, na kufanya mambo kuwa magumu kwetu. Lakini hivyo sivyo jinsi alivyo, Yuko  kwa ajili yetu. Anaelewa vizuri sana mahali  tunapopambana, na anataka kutusaidia mambo yawe bora kwetu.

Ninajuaje kwamba Mungu ananipenda?

Mungu anatuonyesha upendo wake katika Neno lake kwa njia nyingi. Tunapaswa kuamini kile anachosema katika neno lake. Yeye hututunza na anatukumbusha Neno Lake wakati tunapohitaji. Kuna mambo mengi katika maisha ambayo hatuwezi kuyatabiri. Mambo mengi ambayo yanabadilika, mambo mengi ambayo ni magumu. Lakini neno lake halibadiliki kamwe. Na tunapolishikilia, tunaanza kuona ni kiasi gani Yeye anatupenda. Anatuonyesha nini cha kufanya! Na daima kuna neno la kutusaidia. Lakini tunapaswa kuwa tayari kusikiliza.

Tunapoomba msamaha, Mungu hutusamehe, na kisha dhambi hiyo huondolewa. Huu ni uthibitisho wa upendo Wake, inatupa amani ya kujua kwamba tunapoenda kulala dhambi zote tulizotenda tayari zimesamehewa . Alifanya hili liwezekane kwa kutuma kilichokuwa  bora kwake, Mwanawe, Yesu, kwa sababu anatupenda sana.

Hakuna kitu chochote tunachohitaji kufanya ili kustahili upendo wa Mungu. Hatupati upendo wa Mungu kama malipo. Kwa hivyo, ikiwa tunabeba mzigo wa hatia baada ya kuomba msamaha, basi hatuamini kile Neno la Mungu linasema. Mwenyezi Mungu amesahau hilo. lazima pia tuendelee na kuwa tayari kufanya mapenzi Yake wakati ujao.

Tunaweza kupambana na hisia za hatia juu ya mambo ya zamani. Wakati mmoja nilihisi vibaya sana juu yangu mwenyewe, na nilisema tu, "Mungu, nisaidie kujiona jinsi Unavyoniona." Kisha akanikumbusha kuwa aliniumba! Yeye ananijua mimi! Ana mipango mizuri sana kwangu. Na ilikuwa ni faraja sana kwangu. na nilitambua kwamba uzito wote huo ulitokana na mawazo yangu mwenyewe; Haya hayakuwa mawazo ya Mungu kwangu. Na ilikuwa msaada mkubwa kwangu kutambua jinsi anavyoniona.

Namna ya Kumpenda Mungu

Tunapoelewa ni kiasi gani Mungu anatupenda, ni kiasi gani Yeye anapendezwa binafsi na sisi  na ni kiasi gani Yeye binafsi ametufanyia sisi , inabadilisha njia tunayofikiria. Hii inabadilisha jinsi tunavyotaka kuishi. Hii inabadilisha maamuzi na vipaumbele vyetu. Ni jambo la vitendo sana, inakuwa sehemu ya jinsi tunavyoishi. Tunapendezwa na kumpendeza. Kwa hivyo, jinsi tunayozungumza na watu wengine, jinsi tunavyotumia pesa zetu, Jinsi tunayotumia muda wetu, yote inapaswa kuonyesha kwamba tunampenda Mungu.

Tunalo neno lake. Imeandikwa katika Yohana 14:15, "Mkinipenda, mtazishika amri zangu." Tunapaswa kufanya kile anachosema katika Neno lake. Na bila shaka, tunaona kwamba hatufanyi kila kitu kikamilifu, kwa sababu tuna asili yetu ya kibinadamu. Lakini nia yetu ni kutii amri zake kila wakati. Na tunapoona mambo ambayo tunaweza kufanya vyema zaidi, tunafanya uamuzi thabiti wa kujiandaa zaidi wakati ujao.

Kumpenda Mungu inamaanisha kwamba tunawapenda watu walio karibu nasi. Mungu yuko mbinguni, lakini kuna watu wengi karibu nasi, na tunaweza kuwa na bidii sana katika kuwabariki na kuwapenda. Kwa hiyo, kumpenda Mungu ni kitu ambacho ni sehemu ya maisha yetu ya kila siku. Ni njia tunayoishi, na inakuwa sehemu ya mawazo yetu zaidi na zaidi.

Amri zake zinatuonyesha upendo wake kwetu  

Amri za Mungu zinaonyesha upendo wake kwetu. Ni njia ya sisi kuishi maisha yenye furaha zaidi iwezekanavyo. Amri zake si nzito, na ni kweli kabisa. (1 Yohana 5:3.) Hatutii amri zake kwa sababu tunapaswa, au kuthibitisha  kwamba tunampenda Mungu. Tunatii amri Zake kwa sababu tunajua kwamba hilo ndilo jambo bora zaidi tunaweza kufanya, na kwa njia hiyo, sisi ni waaminifu kwake anayetupenda.

Hasa kama kijana, unaweza kuhisi kwamba amri za Mungu ni : "Huwezi kufanya hivi, na huwezi kufanya hivyo." Lakini ukweli ni kwamba, maisha yenye furaha zaidi ni kuishi ndani ya ulinzi wa amri hizo, kwa sababu hekima ya Mungu ni kubwa zaidi kuliko yetu, na tunapotii amri hizo, tunalindwa kutokana na matokeo yote mabaya ya dhambi, na kwa kweli tutapitia upendo wa Mungu kwa njia bora zaidi.

Chapisho hili linapatikana katika

Makala hii ni msingi wa mahojiano na Susi awali yalichapishwa kwenye https://activechristianity.org/ na ilichukuliwa na kupewa ruhusa ya matumizi kwenye tovuti hii.

Shiriki