Sababu 6 nzuri sana za kusoma biblia yako

Sababu 6 nzuri sana za kusoma biblia yako

Kwa nini unaswa kusoma biblia yako leo.

12/4/20165 dk

Na Ukristo wa Utendaji

Sababu 6 nzuri sana za kusoma biblia yako

Kuna nguvu kubwa sana katika neno la Mungu. Je, unatumia nguvu hii katika Maisha yako? Je, unasoma Biblia – neno la Mungu?

Hapa kuna sababu 6 kwa nini unapaswa kusoma Biblia yak oleo.

Soma Biblia: inaeleza mapenzi ya Mungu katika Maisha yetu

“Mapenzi ya Mungu ni yapi katika Maisha yangu?” Hakuna mstari wa biblia unaotuambia hasa kazi tunayopaswa kufanya, mahali pa kuishi na nani wa kuoa. Hata hivyo mwongozo wa Biblia, amri na kutia moyo hutupatia ufahamu wa wazi kabisa wa mapenzi ya Mungu kwetu katika kila sehemu ya Maisha yetu.

Paulio anatuambia kwamba “kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho.” 2 Timotheo 3:16. Hii inamaana kwamba inakuja moja kwa moja kutoka kwa Mungu! Je, umewahi kufikiria kuhusu hili? Biblia imehamasishwa na Mungu mwenyewe! Ni neno lake, na lina hekima yake, wema wake, nia yake, hukumu yake, moyo wake. Je, kweli unataka kuelewa mapenzi ya Mungu? Hivyo chukua muda kusoma neno lake mwenyewe!

  1. Soma biblia: ni chakula chetu cha kiroho

Fikiria kwamba inapita siku moja bila kula chochote. Kisha juma. Kisha mwezi. Kadri muda unavyoenda, unakuwa dhaifu Zaidi na Zaidi. Miili yetu inahitaji chakula kuishi. Na ni sawa pia katika Maisha yetu ya kiroho.

Tuna mawasiliano na Mungu kupitia roho zetu. Ni roho yetu itakayoingia katika umilele na inahitaji chakula ili kuwa hai na macho katika mapenzi ya mapenzi ya Mungu. Yesu alisema, “Imeandikwa, mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu.” Mathayo 4:4. Pia alisema, “Roho ndiyo itiayo uzima, mwili haufai kitu; maneno hayo niliyowaambia ni roho, tena ni uzima.”

Ikiwa tunataka kupata uzima na chakula katika roho yetu, tunapaswa kusoma neno la Mungu na kulifikiria. Neno la Mungu ni chanzo cha uzima! Lina msaada wote na hekima. Na tukisoma na kuamini na kulitii, tutashuhudia ukuaji mzuri wa kiroho.

Soma Biblia: Inahukumu mawazo yetu

Imeandikwa katika Waebreania 4:12 kwamba “maana neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga ukatao kuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.”

Kama wanadamu, ni kawaida kutafuta faida zetu wenyewe (Wafilipi 2:21), hivyo si rahisi kwetu kuona tofauti kati ya mema na mabaya – jinsi tunavyoona mambo mara nyingi huathiriwa na maoni yetu, hisia zetu, na uzoefu unaokwenda kinyume na mapenzi mema na makamilifu ya Mungu.

Lakini neno la Mungu linakatiza haya yote. Linatuonesha mahali ambapo tunatafuta faida zetu wenyewe kwa mfano. Na pia linatuonesha kile ambacho ni kweli na sahihi. Je! Neno langu si kama moto? Asema Bwana, na kama nyundo ivunjayo mawe vipande vipande?” Yeremia 23:29. Neno Mungu lina nguvu, limejaa mamlaka na mapenzi ya Mungu. Ni kama moto uteketezao uchafu na nyundo yenye uwezo wa kuangamiza dhambi zote katika asili yetu! Je, hutaki kulitumia neno hili maishani mwako?

Soma biblia: inafundisha kufanya yaliyo sahihi.

Jinsi gani kijana aisafisha njia yake? Daudi aliuliza katika Zaburi 119:9. “kwa kutii akilifuata neno lako.”

Kila andiko lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kuwaongoza, na kwa kuwabaadibisha katika haki; ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema.: 2 Timotheo 3:16-17.

Biblia ina maagizo na msaada wote tunaohitaji ili kuwa na Maisha safi, ya kweli na uadilifu. Inatufndisha jinsi tunavyoweza kumfuata Kristo. Ina maneno na mifano kutoka kwa mashujaa wa Imani.

Soma biblia: Inatupa nguvu kushinda

Baada ya kufanya uamzi thabiti wa kumtumikia Mungu kwa moyo wote na kutomtenda dhambi, bado tutpata uzoefu wa kwamba tunajaribiwa kutenda dhambi. Yakobo anasema kwamba tunajariibiwa na tamaa zetu wenyewe (Yakobo 1:14).

Ni wazi kutoka kwenye biblia kwamba shetani hutumua tamaa hizi za asili nah amu katika asili yetu ya kibinadamu. Hujaribu kutufanya tusitii mapenzi ya Mungu kwa kutupa vitu ambavyo tunajua kwamba tunavitaka kwa asili: heshima, utajiri au Faraja. Hata alimjaribu Yesu, na kumfanya ajiingize kwenye ubinafsi na kiburi.

Lakini kila wakati ambapo Yesu alijaribiwa, alikuwa na jibu. Na kila jibu lilikuwa linatoka katika neno la Mungu. “Yesu akamwambia, tena imeandikwa, usimjaribu Bwana Mungu wako.” Na anasema Zaidi, “Nenda zako shetani; kwa maana imeandikwa, msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake.” Mathayo 4:1-11.

Je! Wewe pia una neno la Mungu la kujibu kwa kila jaribu unalokabiliana nalo maishani? Je, unajijaza neno la Mungu? Paulo anaandika, “Tena ipokeeni………. na upanga wa roho ambao ni neno la Mungu.” Waefeso 6:17. Biblia, neno la Mungu, ni silaha. Ni upanga unaotoa nguvu ya kushinda katika majaribu. Kwa nini usichukue upanga huu leo?

Soma biblia: imejaa ahadi za Mungu.

Na mwisho,Biblia imejaa ahadi nzuri ajabu. Inazungumza juu ya mambo yote ambayo tutapokea tunapomcha Mungu!

Yeye aliye na sikio, na asikie neno hili ambalo roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye, nitampa kula matunda ya mti wa uzima, ulio katika bustani ya Mungu.” Ufunuo wa Yohana 2:7.

Kuna ahadi nyingi katika Biblia kwa wale wanaoishi kulingana na mapenzi ya Mungu. Je, kweli unapendezwa na ahadi hizi za ajabu? Je, unataka kuona kile ambacho Mungu anafanya na atafanya kwa wale wanaoishi kulingana na mapenzi yake? Kisha soma biblia yako! Itakuambia kuhusu ahadi zote ambazo unaweza kupata, katika Maisha haya na katika umilele, ikiwa tu unafanya mapenzi ya Mungu

Kwa nini usisome Biblia yako leo?

Jamii
Chapisho hili linapatikana katika

Makala hii imejikita kwenye Makala ya Nellie Owens awali ilichapishwa kwenye https://activechristianity.org/ na imechukuliwa na kupewa ruhusa kutumika katika tovuti hii.