Ungefanya nini ikiwa yesu angekuuuliza uachane na kila kitu?

Ungefanya nini ikiwa yesu angekuuuliza uachane na kila kitu?

Ingekuwa imekwenda tofauti ikiwa mtawala mchanga tajiri angechagua kutoa kila kitu

24/3/20174 dk

Na Ukristo wa Utendaji

Ungefanya nini ikiwa yesu angekuuuliza uachane na kila kitu?

Mara nyingi nimefikiria juu ya hadithi ya “mtawala kijana tajiri” (marko 10:17-22) Alikuwa kijana ambaye alijua sheria na alikuwa mwangalifu kuzishika. Lakini hadithi inaonyesha kwamba alijua moyoni mwake kwamba kuna kitu zaidi anahitaji kufanya ili kuwa mkamilifu. Na wakati yesu alipoielezea alijua nini hasa ilikuwa.

Tunaweza kujifunza mengi kutoka kwa hili. Wakati kijana huyo aliuliza ni nini anahitaji kufanya ili kupokea maisha ya milele na kupiga magoti mbele ya yesu, imeandikwa kwamba yesu alimwangalia na kumpenda. Yesu aliona kwamba kijana huyu alikuwa na moyo mzuri na mkweli, na kwamba kweli alikuwa ameishi maisha mazuri. Kwa hivyo, yesu alimwambia ukweli-unachohitaji ni kutoa kila kitu chako na unifuate. Ulikuwa mtihani wa mwisho kuona ikiwa kijana huyo alimpenda yesu kuliko kila kitu. Lakini hakuweza kufanya hivyo. Alikwenda kwa huzuni, kwa sababu alijua ni kweli na hakuwa na nguvu ya kufanya. Na nina hakika Yesu alikuwa na huzuni pia.

Jinsi ingeweza kumalizika.

Mara nyingi nimefikiria juu ya njia nyingine hadithi hii ingeweza kumalizika. Mtawala kijana tajiri alijua kwamba maneno ya yesu yalikuwa ya kweli. Ikiwa angekaa kwa kwa muda mfupi, akanyenyekea na kumwomba yesu amsaidie ndipo hadithi hii ingemalizika kwa namna tofauti. Angesema “Yesu najua upo sahihi. Nahitaji kuacha kila kitu ninachomiliki na ninataka nikufuate; Nahitaji niwe mwanafunzi wako,” hivyo nina hakika yesu angemsaidia.

Yesu aliahidi kwamba ikiwa angetoa mali zake za kidunia, angepata hazina mbiguni. Ili kufanya hivyo, angehitaji kumtumaini mungu badala ya uwezo na mali yake mwenyewe. Lakini basi angejionea jinsi ambavyo Mungu angempa zaidi ya kile alichokitoa. Angekuwa amepokea furaha ambayo haikutegemea bidhaa zake za kidunia, furaha ambayo inaweza kuja tu kwa  sababu alikuwa akiishi maisha ambayo yalimpendeza Mungu kabisa na kwamba alikuwa na mahali pa milele.

Nadhani sisi sote tunafika wakati huo katika maisha yetu ambapo lazima tuchague kutoa kitu ili kuthibitisha kuwa tunampenda Mungu kuliko kitu chochote hapa duniani. Siyo pesa au mali kila wakati. Labda ni uhusiano, wakati wetu, mipango yetu ya siku zijazo au vitu vingine vingi. Vitu hivi siyo lazima viwe “dhambi,” lakini vinaweza kuwa vitu ambavyo tunataka kujiwekea ingawa tunajua kuwa ni mapenzi ya Mungu kwetu kuachana navyo ili aweze kutuongoza kwenye uzima wa milele. Halafu lazima tuchague kukubali ukweli kwa unyenyekevu na kwa msaada wa Mungu kufanya tunachojua ni sawa.

 

Ni thamani kuachana na kila kitu.

Baada ya kijana tajiri kuondoka na wanafunzi walikuwa bado naye, Yesu alitaja jinsi inavyoweza kuwa vigumu kuachana na kila kitu. lakini katika Marko 10:29, Alizungumzia kuhusu kinachotokea wakati mtu anaacha kila kitu kwa ajili yake. “Nawaambieni hakika, hakuna mtu aliyeacha nyumba au kaka au dada au baba au mama au mke au watoto au mashamba, kwa ajili yangu na kwa injili, ambaye hatapokea mara mia sasa katika wakati huu-nyumba na kaka na dada  na mama na watoto na ardhi, pamoja na mateso-na hakika siku zijazo, maisha ya milele.”

Inaweza kuonekana kama chaguo gumu. kwa fikra zetu inaweza kuonekana kama ulimwengu wetu wote utaanguka. Lakini nimepata uzoefu kwamba ninapofanya ninachokijua ni sawa moyoni mwangu, basi mimi hupata amani kubwa na pumziko, hata katikati ya hali hiyo. Inasema katika Yohana 8:32 “Tena mtaifahamu kweli,nayo hiyo kweli itawaweka huru” Hivi ndivyo inavyokwenda kwa wale ambao ni watiifu wakati roho anawakumbusha  juu ya kitu, wanahisi kuwa wako huru kufanya wanachokijua ni sawa na wako huru kusaidia wengine ambao wamefungwa.

Chapisho hili linapatikana katika

Makala hii inategemea nakala ya Heather Crawford iliyochapishwa hapo awali

https://activehchristianity.org/ na imechukuliwa kwa idhini ya matumizi kwenye tovuti hii