Je, umesikia kuhusu Yesu kama mtangulizi wako? Au labda umesikia juu yake kama Yule ambaye amepitia njia kwa niaba yako?
Neno "mtangulizi" linamaanisha nini? Katika hili, "mtangulizi" inamaanisha mtu anayeenda mbele au anaemtangulia mtu wingine. Kwa hivyo, ikiwa Yesu ndiye mtangulizi wetu, lazima kuwe na wengine wanaomfuata, vinginevyo haifai kwake kuitwa "mtangulizi".
“Tuliyo nayo kama nanga ya roho, yenye salama, yenye nguvu, yaingiayo hata mle mlimo ndani ya pazia, alimoingia Yesu kwa ajili yetu, mtangulizi wetu, amekuwa kuhani mkuu hata milele kwa mfano wa Melkizedeki..”Waebrania 6: 19-20.[LS1]
Kumfuata mtu kunapaswa kumaanisha kuenenda katika njia ile ile aliyoenenda , kupata matokeo sawa na aliyopata. Tunamfuataje Yesu? Kwanza, tunapaswa kuelewa Yesu alichotimiza duniani, na kwa nini tungetaka kumfuata.
Yesu alikuwaje Mtangulizi wetu?
Yesu alipozaliwa ulimwenguni, hali haikuwa Kama kipindi cha Adamu kabla ya anguko , bila dhambi na tamaa kamili katika asili yake ya kibinadamu. Badala yake, alianza Maisha yake kama mwanadamu na kama mtumishi, sio Kama mfalme, kwa sababu wakati huo wengi wetu tusingeweza kumfuata. (Wafilipi 2: 7) Alishiriki katika Mwili Na Damu sawa– katika asili ile ile ya dhambi ya kibinadamu - kama watoto. (Waebrania 2:14;Warumi 7: 18.)
“Na, ingawa ni Mwana, alijifunza kutii kwa mateso hayo yaliyompata .”Waebrania 5: 8. Yesu alipaswa kujifunza utii; hiyo ilimaanisha kwamba alikuwa na mapenzi ya kibinafsi ambayo yalikuwa kinyume cha Mapenzi ya Mungu. Yesu alilazimika kuteseka kumtii Baba yake -kutokubali mapenzi yake mwenyewe kulisababisha Mateso. Kila wakati Yesu alijaribiwa kwa dhambi ambayo iliishi Katika mwili wake, katika asili yake ya kibinadamu, Mungu Alilaani dhambi ambayo iliishi huko, na Yesu alikuwa mtiifu. (Warumi 8: 3-4.) Kamwe hakutenda dhambi, lakini badala yake aliiona dhambi iliyoishi Katika Asili yake ya kibinadamu na kuiua kwa kutoikubali mara moja. (Waebrania 4: 15.) Kwa njia hii, dhambi zote na mapenzi ya kibinafsi katika Asili yake ya kibinadamu yaliuawa, na asili ya kimungu ikachukua nafasi katika maisha ya Yesu.
Yesu alipokufa msalabani Kalvari, pazia la hekalu lilipasuliwa vipande viwili kutoka juu hadi chini. (Mathayo 27:51.) Pazia lilikuwa pazia ambalo lilizuia mlango wa kuingia Mahali Patakatifu pa Hekalu na ni ishara ya dhambi katika mwili(katika asili ya mwanadamu) ambayo watu wote wamerithi tangu anguko. Kwa sababu hii ni dhambi inayotutenganisha na Mungu na kutuzuia kwenda mahali patakatifu pa Patakatifu Zaidi. Pazia lilipopasuliwa vipande viwili, lilionyesha kwamba dhambi zote katika mwili wa Yesu (asili ya mwanadamu) zilikuwa zimehukumiwa na kuletwa katika kifo. Yesu alifanya njia mpya na hai kupitia mwili - pazia - hadi kwenye kiti cha enzi cha Baba. (Waebrania 10: 19-22. ) Alikuwa Mtangulizi, na sasa alikuwa ametuwezesha kushiriki kikamilifu katika asili ya kimungu, ikiwa pia tuko tayari kupitia njia ile ile kwa kuweka dhambi katika asili yetu ya kibinadamu katika kifo.
Tunamfuataje Yesu?
“Basi kwa kuwa Kristo aliteswa katika mwili wake, ninyi nanyi jivikeni silaha ya nia ile ile; kwa maana yeye aliyeteswa katika mwili ameachana na dhambi.…”1 Petro 4: 1-2. Yesu ametuonyesha njia kwa kuwa wa kwanza kupigana dhidi ya dhambi ndani Yake, katika asili Yake ya mwanadamu, wakati wake hapa duniani. Ikiwa haikuwezekana kwa mtu yeyote kushiriki katika asili ya kimungu, basi maisha na kifo cha Yesu kingekuwa bure.
Watu wengi wanafikiri kwamba ikiwa wamekuja kwa Yesu, wameenenda katika njia yote. Lakini kuna tofauti kati ya kuja kwa Yesu (ambaye ni Njia) na kwenda njiani mwenyewe.
Inamaanisha nini kuendelea na njia hii kupitia mwili wetu (asili yetu ya kibinadamu yenye dhambi)? " Kwa maana najua ya kuwa ndani yangu, yaani, ndani ya mwili wangu, halikai neno jema; kwa kuwa kutaka nataka, bali kutenda lililo jema sipati..." Warumi 7:18 . Hii ilikuwa asili ile ile ya kibinadamu ambayo Yesu alirithi kama Mwana wa Adamu. Tunapojaribiwa, ni kwa sababu ya dhambi inayoishi katika asili yetu ya kibinadamu, ambayo pia tumerithi kutoka anguko. Ni pale tunapojaribiwa ndipo tuna nafasi ya kuweka dhambi tunayoona ndani yetu katika kifo. Tunafanya hivyo kwa kusema hapana, kwa kutokubali majaribu, lakini badala yake "kujitolea" wenyewe kufanya kile kinachompendeza Mungu. Kwa njia hii, dhambi katika asili yetu ya kibinadamu inauawa kidogo kidogo na kupoteza nguvu zake. Hii ndio maana ya kulaani dhambi katika asili yetu ya kibinadamu. (Warumi 8: 3.)
Yesu Alitoa Mwili wake kama dhabihu ya kufanya mapenzi ya Baba alipokuwa hai. (Waebrania 10: 7[LS9] ; Luka 22: 42.) Ikiwa tunataka kumfuata Yesu, Tunapaswa pia kujitoa kabisa kufanya Mapenzi ya Mungu. Dhambi zetu zimesamehewa Kwa damu ya Yesu , lakini tunapojitoa kabisa kabisa kwa kufanya mapenzi ya Mungu, tunaweza kuingia Sehemu takatifu zaidi Katika damu ya Yesu. Kwa kusema kwa mfano hii ni sawa na damu ambayo pia inapita katika maisha yetu wenyewe tunapoyachukia maisha yetu - mapenzi yetu wenyewe - ili yafe.
Msaada wa kibinafsi kutoka kwa Mtangulizi wetu
Ni katika Mahali patakatifu zaidi ambapo Mungu anajidhihirisha kwetu na anazungumza nasi. Hapa Baba anatuonyesha mapenzi yake ni nini. Hapa pia tunapata kiti cha enzi cha neema. (Waebrania 4: 16.) Hapa ndipo Yesu alipo, mkono wa kuume wa Baba, akiomba kwa ajili yetu. (Waebrania 7: 25 .)“ Na kwa kuwa mwenyewe aliteswa alipojaribiwa, aweza kuwasaidia wao wanaojaribiwa.”Waebrania 2:18. Kwa sababu Yesu alikuwa ameenenda hivi Mwenyewe, na alikuwa amejaribiwa kwa kila namna kama sisi, Anaelewa kile tunachopitia na anaweza kuwa na huruma na udhaifu wetu. (Waebrania 4: 15[LS15] .) Sio huruma ambayo inatuwezesha kuendelea Na dhambi, lakini msaada wa kweli kutoka katika nguvu ambayo dhambi inayo juu yetu na kutoka katika taabu na kifo inachosababisha! Tunapomwomba, huona hitaji letu, na anaomba kwa niaba yetu kwa Baba.
Tunaweza kwenda kwenye kiti cha enzi cha neema ili tuweze kupata neema na msada ili kushinda dhambi kwa wakati unaofaa. Tunahitaji msaada huu ili tuweze kushinda dhambi kama Yesu alivyofanya. Neema hii, ambayo ni msaada kwa wakati unaofaa, sio msamaha baada ya kutenda dhambi, lakini neema na nguvu wakati wa majaribu, ili tusianguke na kutenda dhambi!
Ikiwa tutamchukua Yesu kama Mtangulizi wetu na kuacha mipango yetu yote, na kumfuata na kuwa mwanafunzi wake, basi Yesu pia atakuwa rafiki yetu wa karibu zaidi, wa kibinafsi zaidi. Kupitia Roho Mtakatifu, anazungumza nasi mioyoni mwetu, na anatupa maagizo na ushauri wa kina sana, wa uaminifu na mzuri. Kama Rafiki, Yeye pia hutupa faraja na nguvu na haogopi kutuambia ukweli kamili juu ya jinsi tulivyo, ili tujione na tuweze kubadilika.
Halafu pia tunamwona Yesu kama mtu ambaye sio tu alifanya njia, lakini pia anakimbia pamoja nasi, na moyo uliojaa utunzaji, upendo, tumaini na rehema, akituongoza na kutusaidia kuelekea lengo - ambalo ni kuwekwa huru kutoka katika dhambi katika asili yetu ya kibinadamu ili tu matunda ya Roho yakue na kuonekana ndani yetu!