Kwa nini watu wanaamini kitabu cha miaka 2000?

Kwa nini watu wanaamini kitabu cha miaka 2000?

Biblia inasema nini ambacho kinaweza kutusaidia hata leo?

3/4/20154 dk

Na Ukristo wa Utendaji

Kwa nini watu wanaamini kitabu cha miaka 2000?

Je, Biblia ni ya kweli? Je, Biblia bado inafaa kwa wakati wetu?

Watu wengi wangekubali kwamba maneno kama vile “mpende jirani yako kama nafsi yako” na “kuwa mwenye fadhili na upendo ninyi kwa ninyi, na kusameheana” ni miongozo mizuri ya kufuata. Lakini dini zingine pia zinafundisha mambo yale yale. Kwa hiyo Biblia inasema nini ambacho ni tofauti sana, na je, hiyo inaweza kutusaidia katika maisha yetu leo?

Je, Biblia ni ya kweli, na bado inafaa leo?

Tatizo letu kubwa kama wanadamu ni dhambi, na Biblia inatuonyesha njia ya kuondoa dhambi. Ni mapenzi yetu binafsi, ambayo yanakwenda kinyume na mapenzi ya Mungu, ambayo hufanya mambo kuwa magumu sana. Fikiria maneno makali ambayo Yesu alisema katika Mathayo 5:29, “Jicho lako la kuume likikukosesha, ling’oe ulitupe mbali nawe; kwa maana yakufaa kiungo chako kimoja kipotee wala mwili wako mzima usitupwe katika jehanamu.”

Yesu hakumaanisha kwamba watu wanapaswa kujidhuru, bali alitaka waone jinsi dhambi ilivyo mbaya. Hiyo ilikuwa kweli wakati wa Yesu na bado ni kweli katika wakati wetu ambapo kuna uchafu mwingi kila mahali. Hali zetu zimebadilika, lakini asili yetu ya kibinadamu ni sawa, na ni asili ya kibinadamu ambayo Biblia inaweza kutusaidia.

Roho ya nyakati

Leo, dhambi nyingi zimekubalika na za kawaida, kama uzinzi, uchafu, uchoyo, ubinafsi. Fikiria uchafu wote kwenye televisheni, katika filamu na kwenye mtandao, na shinikizo la kuwa tajiri na mkuu katika ulimwengu huu!

Je, lolote jema linaweza kutoka kwa kufuata “roho hii ya nyakati”, kwangu binafsi au kwa jamii kwa ujumla? Hapana, ni kinyume chake! Je, ni familia ngapi zimeteseka kwa sababu ya ukosefu wa uaminifu hapa? Leo watu wanaweza hata kufikiria kuwa ni jambo la ajabu usipokubali majaribu haya ya uchafu na ubinafsi ambayo yanasemwa wazi dhidi ya Biblia!

Biblia inatuambia jinsi tunavyoweza kupata nguvu za kupinga majaribu haya na kuwa huru kabisa na wasafi!



Maisha ya Yesu

Katika Biblia tunasoma juu ya Yesu, ambaye alituwezesha kuishi maisha bila dhambi. “Ilimbidi kufanywa kama wao, mwanadamu kamili katika kila njia.” Na “alijaribiwa katika kila namna kama sisi. Lakini hakutenda dhambi.” Hii tunaweza kusoma katika Waebrania 2:17 na katika Waebrania 4:15. Hakutenda dhambi hata kidogo, ingawa alijaribiwa kwa kila njia kama sisi!

Yesu alikufa kama Mwana-Kondoo asiye na doa wa Mungu kwa ajili ya ondoleo la dhambi zetu, lakini si hilo tu alilofanya kwa ajili yetu. Pia aliacha nyayo ambazo tunapaswa kuzifuata, kama inavyosomwa katika 1 Petro 2:21, “Kwa sababu ndio mlioitwa; maana Kristo naye aliteswa kwa ajili yenu, akawaachia kielelezo, mfuate nyayo zake.”

Yesu mwenyewe alisema katika Yohana 8:34-36, “Kila atendaye dhambi ni mtumwa wa dhambi… [lakini] Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli.” Na mtume Paulo anatuambia katika Warumi 6:12, “Basi, dhambi isitawale ndani ya miili yenu ipatikanayo n amauti, hata mkazitii tamaa zake. Je, unataka uhuru huu au unataka kubaki mtumwa wa dhambi?

Utachagua nini?

Je, unakuwa na wasiwasi au hofu kwa urahisi? Je, mara nyingi unakuwa na hasira au wivu? Je, unaendelea kufikiria mara kwa mara mambo ambayo mtu fulani alisema au yaliyokuumiza? Je, unapambana na mawazo machafu? Biblia inaweza kukusaidia kuwa huru ili maisha yawe mepesi.

Inawezekana kubadilika unapoweka imani yako kabisa katika Neno la Mungu. Unapaswa kuacha kila kitu, mapenzi yako binafsi, mipango yako ya ubinafsi, lakini unapata kila kitu. Watu ambao walikuwa wakilalamika kila mara, huwa wamejaa shukrani. Mtu ambaye hataki kushiriki anakuwa mkarimu. Mwongo anakuwa mwaminifu.

Je, kweli unataka kuishinda dhambi? Na uko tayari kuacha kila kitu ili kuipata? Hivyo chagua kuamini kwamba maneno yaliyoandikwa katika Biblia ni ya kweli na yanafaa kwako, na fanya kile ambacho Biblia inasema - na maisha yako yatabadilika!

Chapisho hili linapatikana katika

Makala haya yanatokana na makala ya Peter Cheetham yaliyochapishwa awali kwenye https://activechristianity.org/ na yamebadilishwa kwa ruhusa ya matumizi kwenye tovuti hii.