Kuwa na shukrani katika hali zote

Kuwa na shukrani katika hali zote

"Uwe mwenye shukrani katika hali zote." Tunaweza kufanya hivyo kwa namna gani?

26/11/20152 dk

Na Ukristo wa Utendaji

Kuwa na shukrani katika hali zote

3 dak

Mtume Paulo aliandika maneno haya, “Iweni na shukrani katika hali zote ...” 1 Wathesalonike 5:18.

Angewezaje kuwa mwenye shukrani katika hali zote - gerezani, katika kupigwa, katika kila aina ya hali ambazo watu wengi wangeona za kusikitisha na zisizoweza kuvumilika? Ni kwa sababu Paulo alitumaini kwamba Mungu angemtunza kwa njia bora zaidi (Warumi 8:28) huku yeye mwenyewe akikazia fikira “mambo yaliyo juu ambako Kristo ameketi upande wa kuume wa Mungu.” Wakolosai 3:1.

Imani hufanya iwezekane ‘kuwa na furaha sikuzote’

Siku zote alilenga kutafuta vitu hivyo katika asili yake ya kibinadamu ambavyo havitafaa katika ufalme wa mbinguni—mahali pale ambapo moyo wake ulitamani. Na hali zilipokuwa kinyume naye—kama zinavyotufanyia mara nyingi—aliona jinsi alivyotaka kulalamika au hata kulipa ubaya kwa uovu. Lakini neema aliyokuwa ameipata kwa njia ya imani yake katika Kristo Yesu ilimwezesha kuyapinga mambo hayo mabaya aliyoyaona ndani yake, na kitu kipya na cha milele na cha mbinguni kikaja mahali pake. Ndiyo maana angeweza kushukuru daima.

Paulo aliandika hivi katika barua yake kwa Warumi, “Tunajawa na furaha hata tunapoteseka.” Warumi 5:3. Alikaribisha mateso kwa sababu alikuwa na hakika kwamba kitu cha milele kilikuwa kikiumbwa ndani yake ikiwa tu angeweka imani hai katika Mungu! Alikuwa amepokea imani ambayo ilimpa uwezo wa “kuwa na furaha sikuzote” na kushukuru katika kila jambo, hata kwa yale mambo yasiyopendeza, au ambayo yalionekana kutostahimilika kabisa.

Shukrani zake zilimletea Mungu heshima kikweli! Naye anatuambia tufanye vivyo hivyo: “Iweni na shukrani katika hali zote, kwa maana hayo ndiyo mapenzi ya Mungu kwenu ninyi ambao ni wa Kristo Yesu.” 1 Wathesalonike 5:18. Ndiyo maana Paulo alikuwa na "karamu" moyoni mwake, daima, katika hali zote. Hebu tumfuate Paulo katika hili, alipomfuata Kristo!

Chapisho hili linapatikana katika

Makala haya yanatokana na makala ya Carol Laing yaliyochapishwa awali kwenye https://activechristianity.org/ na yamebadilishwa kwa ruhusa ya matumizi kwenye tovuti hii.