Kwa nini Mungu alitupa uhuru wa kuchagua?

Kwa nini Mungu alitupa uhuru wa kuchagua?

Mungu alitupa uhuru wa kuchagua, kwa sababu anataka tufanye maamuzi yetu wenyewe.

17/11/20123 dk

Na Ukristo wa Utendaji

Kwa nini Mungu alitupa uhuru wa kuchagua?

5 dak

Mungu alipoumba watu, aliwapa kitu cha pekee sana. Aliwapa uhuru wa kuchagua ili waweze kufanya maamuzi yao wenyewe.

Anguko (Mwanzo 3) lilitokea kwa sababu Adamu na Hawa walitumia hiari yao kumsikiliza Shetani. Lakini, tunaweza kutumia hiari hiyo hiyo kuchagua kukubali wokovu ambao Yesu alikuja nao, na kumfuata.

Unavuna ulichopanda

Mungu, ambaye ana uwezo wote na hekima yote, amempa kila mtu uhuru wa kuchagua. Hiyo haimaanishi kwamba  tunaweza kufanya chochote tunachotaka bila matokeo yoyote, kwa sababu ingawa tuna hiari, bado tunawajibika kwa maamuzi tunayofanya. Katika Biblia, mawazo tunayochagua kufikiri, maneno tunayochagua kusema na matendo tunayochagua kuchukua, yanalinganishwa na kupanda mbegu kwenye ardhi. Tunaweza kuchagua kupanda mbegu yoyote tunayotaka, lakini mara tu mbegu inapopandwa, hatuwezi kuchagua tutavuna.

“Msidanganyike, Mungu hadhihakiwi; kwa kuwa cho chote apandacho mtu, ndicho atakachovuna. Maana yeye apandaye kwa mwili wake, katika mwili wake atavuna uharibifu; bali yeye apandaye kwa roho, katika roho atavuna uzima wa milele." Wagalatia 6:7-8.

Kubali hiari ya watu wengine

Kama vile Mungu anavyokubali uhuru wetu wa kuchagua, ni lazima pia tukubali uhuru wa kuchagua wa wengine. Je, hiyo inamaanisha kwamba hatuna wajibu kwa mtu mwingine yeyote? Bila shaka hapana. Hebu fikiria watoto. Ikiwa mtoto ni mdogo sana, wazazi wake hawawezi tu kufikiria, “Naam, watoto wana uhuru wa kuchagua pia, kwa hiyo wanapaswa kuruhusiwa kufanya lolote wanalotaka kufanya.”

Wazazi wanawajibika kwa malezi ya watoto wao. Lakini watoto wao wanapokuwa wakubwa, ni lazima wazazi wapate uwiano unaofaa kati ya uhuru wa kuchagua wa mtoto na jukumu la wazazi la kumlea na kumfundisha mtoto huyo.

Tuna mengi ya kujifunza katika eneo hili. Kwa mfano, kama wazazi, tusiwatawale watoto wetu; na hatupaswi kujaribu kuwageuza kuwa nakala zetu wenyewe. Badala yake, tunapaswa kuwa mifano kwao, kuwa nao mioyoni mwetu, na kuwaombea! Tunapaswa kuendelea kuwasiliana nao na kuwasaidia kuelewa mambo waziwazi, badala ya kufanya iwe vigumu kwao kwa kutumia sheria nyingi.

Paulo kama mfano

Ni sawa na mahusiano yetu na watu wengine. Tunaweza kujifunza mengi tunaposoma jinsi Paulo alivyomtendea Filemoni alipokuwa akimzungumzia Onesimo, mtumwa wa Filemoni aliyekuwa Roma na aliyekuwa  ameokoka. "Kwa hiyo nijapokuwa nina ujasiri katika kristo kukuagiza likupasalo; lakini, kwa ajili ya upendo nakusihi, kwa kuwa ni kama nilivyo, Paulo mzee, na sasa mfungwa wa kristo pia.” Filemoni 1:8-9. Anaendelea: “Lakini sikutaka kutenda neno lo lote isipokuwa kwa shauri lako, ili kwamba wema wako usiwe kama kwa lazima, bali kwa hiari.” Filemoni 1:14.

Kutumikia na kubariki kwa hiari yako mwenyewe

Kukubali hiari ya mwingine pia ni muhimu sana linapokuja suala la kutumikia na kutoa kanisani. Kisha hekima inaweza kutufundisha sheria nzuri kuhusu uhusiano wetu na wenzetu. Kwa upande mmoja, tusitawale kamwe, tusisemezane kwa hasira, au kuwa na matakwa  binafsi. Wakati huo huo, lazima tubebane mioyoni mwetu, tuombeane, tutiane moyo na kusaidiana.

Lengo letu lazima liwe kwamba watu wanapaswa kuchagua kwa hiari kufanya mapenzi ya Mungu, kwamba wanataka kiukweli kufanya mapenzi Yake. Ndipo upendo wao kwa Kristo utawaongoza katika sheria kamilifu ya uhuru, kama ilivyoandikwa katika Yakobo 1:25. Wanapoingia katika sheria hii kamilifu ya uhuru, watataka kuwatumikia na kuwabariki wengine - kutoka moyoni, kwa furaha na kwa hiari yao wenyewe.

Chapisho hili linapatikana katika

Makala haya yanatokana na makala ya Jan-Hein Staal yaliyochapishwa awali kwenye https://activechristianity.org/ na yamebadilishwa kwa ruhusa ya matumizi kwenye tovuti hii.