Ujumbe wa msalaba: ukristo wa vitendo

Ujumbe wa msalaba: ukristo wa vitendo

Maisha mema Zaidi ambayo mtu yeyote anaweza kuishi, mahali popote, wakati wowote. Kama kweli unahitaji.

12/7/20164 dk

Na Ukristo wa Utendaji

Ujumbe wa msalaba: ukristo wa vitendo

7 dak

Neno “Mkristo” linamaanisha “mwanafunzi wa Kristo”, na katika Luka 9:23-24 “Yesu mwenyewe anatuambia linachomanisha: “Mtu yeyote akitaka kunifuata, ajikane menyewe, ajitwike msalaba wake kila siku, na anifuate.” Hii ndiyo maana halisi ya ukristo, na inamhusisha kila mkristo wa kweli, bila kujali umri wao, jinsia, utu, historia au hali.

Yesu alijua alichokuwa akizungumzia

Tunaweza kumfuata Yesu katika hili, kwa kuwa ni kile ambacho yeye mwenyewe alifanya alipokuwa duniai. Kama mwanadamu alijaribiwa (Yakobo 1:12-15). Lakini alisema “Hapana” kwa mambo aliyojaribiwa nayo na alijitweka msalaba kila siku – Hii inamaanisha kwamba hakujitoa kwa dhambi ambazo alijaribiwa nazo, na hivyo kamwe hakutenda dhambi. (Waebrania 2:14; Waebrania 4:15.)

Ni wazi kabisa kwamba Yesu alijua asili ya mwanadamu ilivyokuwa; binafsi alishuhudia ilivyopaswa kuwa kwa mwanadamu na asili ya dhambi. Alitumia mifano hai inayotuonesha kwamba alijua ilivyokuwa kujaribiwa:  Kuwa na wivu, kuwa na uchungu, kuwa na tamaa, kuhukumu, kuwa na wasiwasi, kuwa na majivuno, kuwa mnafiki n.k.

Lakini kila siku kwenye maisha yake, alitumia “msalaba”. Hapa ndipo mahali ambapo tamaa za dhambi katika asili yake ya kibinadamu (ambayo pia huitwa mwili)  zilikutana na kifo. Kwa maneno mengine, hii inamaanisha kwamba kwa nguvu ya Mungu alisema “Hapana” kwa dhambi katika asili yake ya dhambi mpaka aliposhinda, mpaka pale dhambi aliyojaribiwa nayo ilipokufa.

Kutokujitoa kwa dhambi huleta mateso. Hivyo Yesu alipaswa kuteseka katika mwili, na alimlilia Mungu kwa ajili ya msaaada, lakini pia inamaanisha kwamba hakutenda dhambi. (1Petro 4:1; Waebrania 2:14; Waebrania 5:7)

Kwa kweli tunaacha kutenda dhambi!

“Ujumbe wa msalaba” ni wa vitendo sana. “Msalaba” unaweza kutumika katika maisha ya kila siku, kwa mtu ye yote, bila kujali umri wao, jinsia, utu, historia ama hali. Unaweza kutumika katika hali yo yote, katika jaribu lo lote.

Tunapojitweka msalaba wetu kila siku, hatujitoi kwenye hisia za hasira, uchungu, au wivu. Hatujitoi kwa ajili ya majaribu ya kujivuna au mashtaka au uvivu. Haturuhusu mawazo machafu. Tunakataa kujionea huruma wenyewe au kukatishwa tamaa ambako kunaweza kutuzuia kutenda mema. Tunaanza kutenda neno la Mungu. (Yakobo 1:21-22)

Kwa kutumia msalaba “tunaziua” tamaa za dhambi katika asili yetu kabla hazijakua dhambi. (Yakobo 1:14-15; Wakolosai 3:5; Wagalatia 5:24.)  Hii inamaanisha kwamba hatukubali dhambi mpaka pale dhambi inapokufa ndani yetu. Paulo anasema kwamba ujumbe wa msalaba ni nguvu ya Mungu kwa wale waaminio, na hiyo ndio hekima ya Mungu. (1Wakorintho 1:18-25) Tunaliona hili katika mazoezi! Kwa kutumia msalaba na nguvu kutoka kwa roho mtakatifu, tunabadilika.

Tulipokuwa na uchungu na wakali awali, tunakuwa baraka. Tulipokuwa tunaogopa na kukata tamaa, tunajazwa na Imani na nguvu ya kutenda. Pale tulipokuwa tunakosoa na wenye chuki, tunajifunza kusamehe na kujenga. Badala ya kugombana pale ambapo hisia zetu zimeumizwa au maoni yetu yanapokataliwa, tunakuwa mfano katika upole, wema na uvumilivu. Kama tunavyosema “Hapana” kwa tamaa zetu za dhambi, tunapata matunda ya roho zaidi na Zaidi.

Matokeo ya ajabu

Ni furaha kiasi gani kwa familia zetu, marafiki zetu na wafanyakazi wenzetu tunapoacha kuwa wakali na kuwa wapole, wenye shukranni badala ya kuwa wenye uchungu, wachangamfu badala ya kuwa wenye huzuni. Ni unafuu kiasi gani tunapoacha kuwa mabosi na badala yake kuanza kusaidia wengine. Ni baraka gani kwa jamii ambapo wavivu wanakuwa wanafanya kazi kwa bidi, na ambapo watu wengi Zaidi wanakuwa wenye haki, wakweli na waaminifu.

Kama wakristo tunakuwa mifano ya haki, huruma, na kwa kila jambo ambalo ni haki na jema. Sisi ni nuru ambayo haiwezi kufichwa. (Mathayo 5:14-16) Popote tulipo, chochote tunachokutana nacho, kwa namna yoyote tunavyohisi, kwa hali yoyote, yeyote tuliye nae, ujumbe wa msalaba utafanya kazi, na kuzalisha matokeo mema. Ni ukristo katika vitendo.

Chapisho hili linapatikana katika

Makala hii imejikita kwenye Makala ya Milenko Van der Staal awali ilichapishwa kwenye https://activechristianity.org/ Imechukuliwa na kupewa ruhusa kutumika kwenye tovuti hii.