Upendo wa ubinafsi au upendo wa Mungu: Upi ulionao?

Upendo wa ubinafsi au upendo wa Mungu: Upi ulionao?

Zipi ni sababu na matokeo ya upendo wangu? Nina upendo ambao unafikiri tu kuhusu mimi binafsi au wenye kuleta uzima, upendo usio na ubinafsi?

2/11/20183 dk

Na Ukristo wa Utendaji

Upendo wa ubinafsi au upendo wa Mungu: Upi ulionao?

Upendo wa ubinafsi.

Upendo wa ubinafsi ni kuhusu “Mimi’’, “Mwenyewe” na “Yangu”. Mtu ambaye upendo wake ni kumhusu yeye kama buibui katikati ya utando wake, akishikilia Kamba zote kwenye mikono yake. Kila kitu ni kumhusu yeye. “Mimi” ni mfalme, “Mimi” ni mungu, “Mimi” lazima nipendwe, niheshimiwe na kusifiwa – vinginevyo utahisi hasira “yangu”. “Mimi” siwezi kutoa chochote bure. “Mimi” lazima kwanza kuwa na uhakika kwamba “Mimi” nitalipwa kiasi chote kabla ya kufanya kitu. “mimi” ninahitaji kila kitu na nina haki kwenye kila kitu.

Upendo wa ubinafsi huweka jitihada zote kwenye “Mimi” ninataka. Hakuna jitihada yeyote inayotoka kwenda kwa wengine. Ni kama kuhusu Mimi mwenyewe.

Upendo wa Mungu

Upendo wa Mungu huacha jua lake liangaze kwa wenye haki na wasio haki. Hutuma mvua kwa waovu na wema. Wema wake wote humiminika- hakuna kitu kizuri sana kutopewa. Kama vile jua linavyoangaza bila upendeleo kwa kila mtu, hivyo ndivyo upendo wa Mungu unavyoangaza kwa uangavu na u-joto na hutupa kila kitu tunachohitaji kuishi maisha ya ki-mungu. (2 Petro 1:3).

Upendo wa ubinafsi huharibu

Mtu ambaye amejazwa pendo la ubinafsi hujijali mwenyewe. Kila kitu ni kumhusu yeye. Kwa sababu hajali kuhusu vitu na watu wanaomzunguka, muda kidogo huwa muhanga wa nguvu yenye kuharibu inayotokana na upendo wa ubinafsi – ambao ni Shetani mwenyewe. Upendo wa ubinafsi humtega muhanga na kuharibu kwa namna ya kutisha.

Upendo wa Mungu hutoa na kutengeneza maisha

Roho mtakatifu amemimina upendo wa Mungu kwenye mioyo yetu. Upendo huu daima kuangaza njia kuifanya nzuri kwa wengine. Upendo wa Mungu hutupa dunia yote kuifanyia kazi, lakini upendo wa ubinafsi unaweza tu kutafuta mtu mmoja, huyo ni “Mimi’, na hata kuumiza na kuharibu mtu huyo.

Upendo wa Mungu hutazamia kushiriki na kutoa; hutengeneza maisha na furaha popote ulipo. Kila mmoja “Hupenda” upendo huu, lakini upendo wa ubinafsi huchukiwa kila mahala.

Ikiwa tunataka kusaidia watu, lazima tuweze kuona wanachohitaji. Tunaposaidia watu bure na bila ubinafsi, huwashangazwa sana. Wanapata kuangalia kidogo kwa upendo ambao hutoa na hauhitaji chochote kwao. Upendo huu ni tofauti kabisa na upendo wa duniani ambao wameuzoea. Ndio maana imeandikwa kwamba wema wa Mungu hutuongoza katika huzuni juu ya dhambi na majuto. Tunapata upendo ambao huja kutoka nje yetu-ambao ni mkuu kuliko upendo wa ubinafsi.

Upendo huu una matokeo ya kushangaza: Watu ambao wanapata upendo huu, pia wanataka kuwa nao. Upendo wa Mungu hupanda kitu fulani cha asili yake (kimungu) ndani yetu. Tunageuka kutoka kwenye upendo wa ubinafsi kwenda upendo wa kimungu na kisha tunataka kutenda na kushiriki vitu vyote ambavyo upendo wa Mungu umetupatia.

Kushiriki hazina ya mbinguni

Mtu ambaye ni tajiri katika dunia hii anaweza, ikiwa ni mpole, kutenda wema na kuleta furaha kwa watu wengi. Kwa njia ileile, mtu ambaye amejikusanyia utajiri katika Bwana anaweza kutumia utajiri wake kuleta furaha kwa wengi. Ikiwa utajiri wa dunia unaweza kuwafanya watu kuwa na furaha kwa muda katika dunia hii, kwa kiasi gani utajiri wa mbinguni unaweza kuwa na thamani zaidi ambao unaweza kutufanya kuwa na furaha kwa umilele wote.

Utapata upendo wa Mungu pale unapotaka kuwa nao kwa moyo wako wote. Tumeshaupokea bure, na tunaweza kuushiriki na wengine bure.

Chapisho hili linapatikana katika

Makala hii imejikita katika Makala ya Johan Oscar Smith ambayo awali yamejitokeza yakiwa na kicha “Upendo ni nini?” Katila jarida la BCC “Skjutter” (Hazina iliyofichwa) Septemba 1917. Imetafsiriwa kutoka kwenye Kinowei  na  imebadilishwa kwa ruhusa kutumiwa kwenye tovuti hii.