Alitumwa kama mtumishi wa Mungu

Alitumwa kama mtumishi wa Mungu

Mungu alipomtuma Mwanawe duniani kuwa Mwokozi wetu, alimtuma kuwa mtumishi wake.

20/1/20262 dk

Written by Helen Simons

Alitumwa kama mtumishi wa Mungu

Nabii Isaya anaandika: " Tazama mtumishi wangu nimtegemezaye; mteule wangu, ambaye nafsi yangu imependezwa naye; nimetia roho yangu juu yake; naye atawatolea mataifa hukumu..'" Isaya 42: 1.

Katika kumtumikia Baba yake, Yesu pia akawa mtumishi wetu. Ungefikiri kwamba mtu ambaye Mungu aliyemtuma kuwa Mwokozi wetu na Mfalme wetu angefika katika utukufu mkubwa ili ulimwengu uone mara moja Yeye ni nani na alikuja kwa nini! Lakini Biblia inasema, " bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu." Wafilipi 2: 7.

Asili ya mwanadamu kimsingi ni ya ubinafsi, na kwa kawaida watu hufikiri kwamba ikiwa wengine watawahudumia na kuwatendea vizuri, watakuwa na furaha. Lakini furaha ya kweli ina chanzo kirefu zaidi kuliko hicho! Yesu alisema, " Lakini mimi kati yenu ni kama atumikaye.." Luka 22:27. Alionyesha hili kwa mfano wake mwenyewe. Pia anasema juu yake mwenyewe, " kama vile Mwana wa Adamu asivyokuja kutumikiwa, bali kutumika, na kutoa nafsi yake iwe fidia ya wengi." Mathayo 20:28.  

Yesu hakuwatumikia wengine ili kuheshimiwa nao, lakini kwa sababu aliwapenda. Alichagua hasa kuwatumikia wale ambao hawakuweza kufanya chochote kwa ajili yake, kama watoto wadogo, viwete na vipofu, wenye ukoma na waliotengwa. Wote wangeweza kuja kwake ili kufarijiwa na kuponywa. Yesu aliwatumikia kwa sababu aliwapenda watu, sio kwa sababu walistahili.

Sio sawa kutumika na kutenda mema tu kwa wale ambao tunafikiri wanastahili. Yesu alipenda kutenda mema na alichukia udhalimu, na ndiyo sababu Mungu alimtia mafuta " Mafuta ya shangwe kupita wenzie", kama Biblia inavyosema katika Waebrania 1: 9. Kwa maneno mengine, Alikuwa mtu mwenye furaha zaidi kuwahi kutembea hapa duniani!

Sasa ni zamu yetu! Tuna nafasi ya kufuata nyayo za Yesu na kuwatumikia wengine kupitia upendo. (1 Petro 2:21; Wagalatia 5: 13-14.) Ikiwa tunampenda na kumtumikia Mungu, atatuonyesha pia namna bora ya kuwatumikia wanadamu wenzetu!

Chapisho hili linapatikana katika

Makala hii inatokana na makala ya Helen Simons iliyochapishwa awali kwenye https://activechristianity.org/ na imebadilishwa kwa ruhusa ya matumizi kwenye tovuti hii.