Acha kuwa na mawazo duni juu ya Mungu!

Acha kuwa na mawazo duni juu ya Mungu!

Je, kweli unaamini katika wema na nguvu za Mungu? Au unafikiri Mungu ni dhaifu kama wewe?

29/6/20183 dk

Na Ukristo wa Utendaji

Acha kuwa na mawazo duni juu ya Mungu!

Tunapaswa kuwa na mawazo ya chini juu yetu wenyewe, lakini mawazo makuu juu ya Mungu na kile anachoweza kufanya ndani yetu! Yeye ni Mwalimu mkuu sana na mzuri na mwenye nguvu! Anaweza kufanya jambo la kushangaza, hata kwa watu dhaifu sana!

Acha kuwa na mawazo duni juu ya Mungu!

Unafanya makosa makubwa sana unapofikiri ni unyenyekevu kuamini kwamba Mungu hawezi kufanya mengi ndani yako na kupitia kwako. Halafu unafikiri Mungu ni sawa na wewe. Badala ya kuwa na mawazo duni juu yako mwenyewe, una mawazo duni kuhusu Mungu - ambayo ni tofauti kabisa na kuwa mnyenyekevu!

Ikiwa tungelazimika kujaribu sisi wenyewe kuwa kama Yesu haswa, itakuwa sawa kabisa kufikiria kuwa haiwezekani. Lakini kujaribu peke yetu ni kosa kubwa sana! Ni Yeye Mwenyewe—Bwana mkuu na mwema—ambaye atatubadilisha na anaweza kutubadilisha.

“Umkabidhi Bwana njia yako, pia mtumaini, naye atafanya.” Zaburi 37:5. "Yeye ni mwaminifu ambaye awaita, naye atafanya." 1 Wathesalonike 5:24.

Amini kwamba Mungu ni mwema kama alivyo kweli!

Tunaweza kusema kwamba jambo gumu kuliko yote ni kuamini kwamba Mungu ni mwema kama Yeye alivyo. Hatuna shida kuamini kwamba Mungu ni mwema na kwamba anatusamehe dhambi zetu. Lakini kuamini kwamba Yeye ni mwema sana kiasi  kwamba atatuacha tushiriki tabia yake ya kimungu, kwamba atatufanya tuwe washindi juu ya kila dhambi tunayoweza kufikiria, na pia kwamba atatutumia na kutukabidhi mambo makuu - hii ni ngumu sana kuamini.

Lakini tunapaswa kufanya nini? Tunapaswa kuamini kile ambacho Biblia inasema! Kuamini ahadi zote zilizoandikwa hapo! Kwa mfano:

Wakolosai 1:28: “ambaye sisi tunamhubiri Habari zake tukimwonya kila mtu, na kumfundisha kila mtu katika hekima yote, tupate kumleta kila mtu mtimilifu katika Kristo..”

Wafilipi 1:6  - nami niliaminilo ndilo hili, ya kwamba yeye aliyeanza kazi njema nioyoni mwenu ataimaliza hata siku ya Kristo Yesu..

Wafilipi 2:15: “Mpate kuwa wana wa Mungu wasiokuwa na lawama, wala udanganyifu, wasio na ila kati ya kizazi chenye ukaidi, kilichopotoka, ambao kati ya hao mnaonekana kuwa kama mianga katika ulimwengu."

Wafilipi 4:13  - “Ninayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.”

Waefeso 3:19-20: “…mpate kutimilika kwa utimilifu wote wa Mungu.

Hebu tusome mstari huu wa mwisho tena: “…mpate kutimilika kwa utimilifu wote wa Mungu.” Ndiyo, ni nani anayeamini kwamba Mungu anaweza na atafanya mambo makubwa kama hayo? Je, unafikiri kwamba ni fahari kuamini kwamba Mungu anaweza kutupa sisi wanadamu asili yake? Kwa maneno mengine, unafikiri kwamba kuwa na mawazo makuu kuhusu wema wa Mungu na nguvu Zake ni kujivunia? Au labda unafikiri kuwa na mawazo ya chini juu ya kile ambacho Mungu anaweza kufanya ndani yako ni kuwa mnyenyekevu?

Hapana, basi unachanganya kila kitu. hivyo unafikiri kwamba Mungu ni kama wewe - dhaifu na asiye na uwezo. Unapaswa kubadilisha njia hii ya kufikiria!

Chapisho hili linapatikana katika

Makala hii inategemea makala ya Elias Aslaksen ambayo ilionekana kwa mara ya kwanza chini ya kichwa “Uwe na mawazo madogo kukuhusu, lakini mawazo makuu kumhusu Mungu na kuhusu kazi Yake pamoja nawe!” katika jarida la BCC la "Skjulte Skatter" (Hazina Zilizofichwa) mnamo Aprili 1951. Imetafsiriwa kutoka kwa Kinorwe na imechukuliwa kwa ruhusa ya matumizi kwenye tovuti hii.