Haki hutoa thawabu kubwa katika siku zijazo

Haki hutoa thawabu kubwa katika siku zijazo

Je, umefikiria juu ya haki ni nini na ni nini thawabu zake?

7/5/20187 dk

Na Ukristo wa Utendaji

Haki hutoa thawabu kubwa katika siku zijazo

Neno la Mungu na hekima ya Mungu zimejawa na haki. "Lakini kwa Habari asema, kiti chako cha enzi, Mungu, ni cha milele na milele; na fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya adili." Waebrania 1:8 .

Yesu alikuwa mtu mwenye furaha zaidi duniani kwa sababu alipenda haki, kama ilivyoandikwa katika Waebrania 1:9. Haki ni kutenda yaliyo haki machoni pa Mungu. Huleta baraka. Huleta amani na furaha. Ni sheria ya ufalme wa Mungu. Kwa hivyo, kujifunza haki kunatoa thawabu kubwa, kwa maisha haya na milele yote. Haituathiri sisi tu bali watu wanaotuzunguka - jamii tunayoishi.

Hapa kuna baadhi ya thawabu tunazopata ikiwa tutafuata haki kwa mioyo yetu yote:

Furaha ya kujua nini kinakuja

Kuwa mwadilifu ni kutenda yaliyo mema na mazuri machoni pa Mungu. Mwanzoni, inaweza kuonekana kama kufanya haki ni hasara, lakini kwa muda mrefu, kuna thawabu kubwa.

Fikiria maisha ya mtu ambaye anataka kuwa mchezaji wa mpira wa miguu. Anajua kwamba anapaswa kufanya mazoezi fulani na kula vyakula fulani vyenye afya ikiwa atakuwa katika hali nzuri. Hata kama siku fulani anataka kula chochote anachohisi kula, anaamua kutofanya hivyo kwa kuwa anakumbuka lengo lake - kuwa mchezaji mzuri wa mpira wa miguu. Baada ya hapo, alifurahi sana kwamba alifanya uamuzi sahihi. Lakini kama angefanya uamuzi mbaya, angejuta baadaye.

Ndivyo ilivyo katika kila eneo. Haki huleta furaha ambayo huenda zaidi kuliko kipindi kifupi sana cha "shangwe" ambayo tunapata tunapokubali dhambi. Kama sisi daima tutachagua haki, tunaweza kutarajia matumaini ya baadaye (Yeremia 29:11) ambayo ni ya kuvutia zaidi kuliko maisha kamili ya uchaguzi mbaya na kusubiri kwa hofu matokeo ya kutisha ambayo yatapaswa kuvunwa. Matendo ya haki ni uwekezaji kwa ajili ya siku zijazo!

Utulivu kamili na amani ambayo haiwezi kutikiswa

Yesu akawa Mfalme wa Amani, na kabla ya kuondoka duniani, aliwaambia wanafunzi wake , "Amani nawaachieni; amani yangu nawapa; niwapayo mimi sivyo kama ulimwengu utoavyo. Msifadhaike mioyoni mwenu, wala msiwe na woga." Yohana 14:27.

Fikiria wakati Yesu aliposimama mbele ya Pontio Pilato. Inawezekanaje kwamba angeweza kusimama huko katika pumziko kamilifu wakati wote walikuwa wakimshtaki? (Mathayo 27:11-14)) Inawezekanaje kwamba alikuwa anafikiria juu ya mama yake na Yohana, hata alipokuwa akining'inia msalabani? (Yohana 19:25-27) aliwezaje kufanya hivyo?

Siri ilikuwa kwamba alikuwa amepokea amani kwa kuacha mapenzi Yake mwenyewe – vile alivyopennda mwenyewe na asivyovipenda. Kwa Yesu, haki ilikuwa ni kuacha mapenzi yake mwenyewe na kufanya mapenzi ya Mungu. (Waebrania 10:7.) Haki ilikuwa ni kukataa kuchukua heshima yoyote kwa ajili yake mwenyewe, kwa sababu heshima yote ni ya Mungu. Yesu alikuwa mtu mwenye haki zaidi aliyewahi kuishi, na aliteseka kama mwenye haki kwa wasio haki, ambao ni sisi, na kwa kufanya hivyo, angeweza kutuleta kwa Mungu. (1 Petro 3:18.)

Kama wanafunzi, sasa tuna nafasi ya kwenda katika njia ile ile ambayo Yesu alienda, na kwa kumfuata, tunaweza kupata furaha na amani ile ile ambayo Yesu alikuwa nayo - amani ambayo haiwezi kutikiswa na kitu chochote au mtu yeyote katika hali yoyote! (Yohana 15:11))

Unaweza kufikiria, "Mimi ni mwenye haki, kwa sababu mambo yangu yote ya fedha yako sawa. Ninalipa gharama zangu zote." Lakini labda bado umejaa mahitaji au matarajio kwamba wengine wanapaswa kufanya hili au lile. Labda umejaa machafuko kwa sababu ya udhalimu wa watu wengine.

Lakini haki ambayo Yesu alikuja nayo si haki ya kibinadamu. Inakwenda mbali zaidi kuliko haki ya binadamu. Ndiyo maana amani na raha inayotokana na "haki inayotokana na Mungu kwa imani" (Wafilipi 3:9) haiwezi hata kulinganishwa na furaha ndogo inayotokana na kufanya tu yaliyo sawa kulingana na sheria au maadili ya kibinadamu.

Haki ya Mungu ni kufanya yaliyo mema na ya haki machoni pa Mungu, katika maeneo yote. Ninaepuka mafadhaiko mengi kwa njia hii, kwa sababu basi ninaishi kwa kumpendeza Yeye na sihitaji tena kupigania faida zangu mwenyewe. Sihitaji kupigania heshima yangu mwenyewe, pesa, au hata kwa mawazo yangu mwenyewe ya haki. Ni zawadi ya ukombozi! Na malipo yangu ya muda mrefu yatakuwa nini? Mungu anatuambia, "Vema, mtumwa mwema na mwaminifu," kama ilivyoandikwa katika Mathayo 25:23. Kusikia kwamba siku moja, itakuwa ya thamani zaidi kuliko tuzo yoyote ya kidunia tunayoweza kufikiria sasa.

Haki inavunja mapenzi yetu ya kibinafsi ya uharibifu

Uadilifu unamaanisha kwamba hatufanyi mapenzi yetu wenyewe. Lengo la mwanafunzi ni kuwa na mawazo yale yale ambayo Yesu alikuwa nayo:  "Tazama, nimekuja kufanya mapenzi yako, Ee Mungu—kama ilivyoandikwa juu yangu katika Maandiko," na, "Nataka mapenzi yako yatendeke, sio yangu." Waebrania 10:7 (NLT  ) na Luka 22:42 (NLT). Tunaona kutoka hapa kwamba mapenzi yetu ya kibinafsi na mapenzi ya Mungu hayako sawa. Hayana mchanganyiko au mwingliano kabisa. Mapenzi yetu wenyewe yanapaswa kukataliwa ili mapenzi ya Mungu yaweze kufanywa. Hiyo ni haki machoni pa Mungu.

Kujipenda kwetu ni kila kitu kinachoweka "Mimi" kwanza na mara nyingi husababisha madhara kwa mtu mwingine. Haya ndiyo mapenzi tunayozaliwa nayo. Watu wengi kamwe hawawi nje ya hatua hii. Kwa nje, wanaruhusu mambo yaonekane bora kuliko yalivyo. Lakini kwa nini kuna mgogoro? Kwa nini kuna machafuko? Kwa nini kuna vita na matatizo nyumbani na duniani kwa ujumla?

Mapenzi yangu mwenyewe yamejaa udhalimu, bila kujali jinsi ninavyojaribu kuyaficha. Mtu mwingine ana mapenzi yake mwenyewe na nina mapenzi yangu, na kisha nadhani, "Kama ungeweza kufanya  mapenzi yangu tu, basi tunaweza kuwa marafiki wazuri." Lakini wazo hili ni uongo mkubwa. Hapa ndipo ambapo mgogoro unatoka. (Yakobo 4:1-2.) Ubinafsi wa mwanadamu husababisha matatizo mengi duniani.

Ninapoanza kuona mapenzi yangu yalivyo tatizo, kisha kuyakata na kufanya mapenzi ya Mungu inakuwa faida kubwa kwangu na kwa wale walio karibu nami.

Je, unawajali watu? Unataka kufanya mambo mazuri nyumbani kwako, katika jamii yako, au katika jamii unayoishi? Kama ni hivyo, basi kukua katika haki hii – katika kutoa mapenzi yako mwenyewe na kufanya mapenzi ya Mungu badala yake - itakuwa faida kubwa kwa familia yako, majirani zako, marafiki zako, wenzako, ubinadamu kwa ujumla, na maisha yako ya baadaye, katika ulimwengu huu na milele!

Umoja kamili na amani na kila mtu

Hapo awali tuliona kwamba mchezaji wa mpira wa miguu alikuwa na lengo, maono, na hiyo ilikuwa kuwa mchezaji wa soka wa kulipwa. Kwa sisi, maono haya ni kwamba kutoka upande wangu - katika maisha yangu - mgogoro na matatizo kati yangu na watu wengine yanaweza kutatuliwa kabisa kupitia haki, haki ya Mungu.

Ni njia gani ya kuishi! Inawezekana kabisa kuwa nayo kama  hivi: "Kwa upande wangu, kila mtu anaweza kuishi kama alivyo." Unapofikiria juu ya maono ya kuwa mtu ambaye hana mgogoro na mtu yeyote au kitu chochote - bila mgogoro wa ndani na huzuni - basi maono hayo yanatupa uwezo wa kufanya kile kinachohitajika leo, kusema hapana kwetu na kumfuata Yesu. (Luka 9:23))

Haya ni maono yale yale ambayo Yesu alikuwa nayo. Alikuwa ametazama chini ya dunia na kuona vita vyote. migogoro katika nyumba, na migogoro kila mahali. Watu, ambao waliumbwa kuwa kama Mungu Mwenyewe, walikuwa wakikimbia na kuuana, wakikoseana na kuwa wabaya kwa kila mmoja. Ndiyo sababu Yesu alikuja duniani na kuonyesha kwa mfano wake mwenyewe kwamba tunaweza kufanya kazi pamoja kwa amani na umoja ikiwa tutaacha mapenzi yetu ya kibinadamu kufanya mapenzi ya Mungu. (Waefeso 4:1-6; Waefeso 4:11-16Yohana 17:20-23; Waefeso 2:14-161 Yohana 1:6-7.)

Furaha ambayo Yesu alikuwa akitazamia ilikuwa kwamba kutakuwa na kaka na dada wanaoishi pamoja katika umoja kamili. (Waebrania 12:2; Zaburi ya 133.) Kwa watu wengi, tofauti husababisha migogoro moja kwa moja. (Yakobo 3:16; Yakobo 4:1-2.Lakini katika ufalme wa Mungu, tofauti hupelekea amani ambayo haisikiki duniani.

Zawadi kubwa zaidi ya kuchagua maisha ya haki ni ile ambayo  Yesu aliiomba katika Yohana 17: 21-23 - ili tuweze kuwa kitu kimoja kama Baba na Mwana walivyo wamoja. Fikiria juu ya nini kinaweza kufanyika panapokuwa na umoja kamili kati ya watu!

Chapisho hili linapatikana katika

Makala hii inategemea makala ya Eunice Ng iliyochapishwa awali kwenye https://activechristianity.org/ na imebadilishwa kwa ruhusa ya matumizi kwenye tovuti hii.