Nilichukia utu wangu na nilichukia jinsi nilivyofanya kati kati ya watu wengine. Nilichukia jinsi nilivyofanya na kusema mambo. Nilitaka kuwabariki wengine; Nilitaka kuwa aina ya mtu ambaye alionyesha jinsi ilivyo vyema kuwa Mkristo. Lakini sikuweza kwa sababu sikuwa na ujasiri; Sikufikiria kama nilikuwa mwema vya kutosha. Hii ilinizuia kufanya na kusema mambo ambayo Mungu alifanyia kazi ndani yangu kufanya au kunena.
Bila kujua, nilikuwa nikisema, "Sikubaliani na Mungu, ambaye aliumba vitu vyote, na ambaye pia aliniumba." Aliniumba kama nilivyo, na utu wangu, karama zangu, na sura yangu; na kimsingi nilikuwa nikisema kwamba aliniumba vibaya. Nilipogundua hili, niliona kwamba kwa kweli ilikuwa dhambi kuwa na mawazo haya ya chini na hasi juu ya jinsi Mungu alivyoniumba. Ilikuwa ni kutokuwa na shukrani, na kutoamini kwamba Mungu alikuwa na mpango kamili kwa ajili yangu, kama vile alivyoniumba.
Nilisoma katika Neno la Mungu juu ya tunda la Roho, juu ya upendo, furaha, amani, uvumilivu, fadhili, wema, uaminifu, upole, kiasi na nilijua kuwa hili ndilo nilitaka sana katika maisha yangu.
Chombo mikononi mwa Mungu
Nilimwomba Mungu kwamba anisaidie kujiona jinsi alivyoniona. Kwa msaada wake nilianza vita vya ndani kushinda kutokuwa na shukrani ndani yangu - dhambi hii, kwa kuwa ni dhambi kutoshukuru kwa jinsi Mungu alivyoniumba. Kwa kweli, Mungu hakuondoa tu mawazo haya yote hasi juu yangu mwenyewe. Lakini yalipokuja basi alinipa nguvu ya kupigana nayo.
Nilishikilia mstari katika 1 Wakorintho 6:20: " maana mlinunuliwa kwa thamani. Sasa basi, mtukuzeni Mungu katika miili yenu." Kila wakati nilipojaribiwa kuwa na mawazo ya chini, hasi juu yangu mwenyewe, nikasema "Hapana. Mungu alininunua kwa thamani. Aliona kitu cha thamani ndani yangu." Kujihisi duni kulinifanya nisiwe na msimamo. Mawazo haya hasi hayakuwa ya kweli, na yalinizuia kumtukuza Mungu katika mwili wangu na roho yangu, ambayo ni ya Mungu.
Dhambi huleta machafuko na taabu. Nilipata uzoefu huo mwenyewe. Lakini ninaposhinda dhambi ninaweza kupumzika na kuwa na furaha katika maisha yangu. Ninapoishi maisha ya kushinda ninaweza kuwa chombo mikononi mwa Mungu (Warumi 6:13), na anaweza kunifundisha na kunitumia kama anavyotaka.