Kipi ninapaswa kukumbuka kuhusu “siku mbaya”

Kipi ninapaswa kukumbuka kuhusu “siku mbaya”

Ulishawahi kuwa na siku ambapo kila kitu kilionekana kwenda tofauti?

2/5/20162 dk

Na Ukristo wa Utendaji

Kipi ninapaswa kukumbuka kuhusu “siku mbaya”

3 dak

Ulishawahi kuwa na siku ambapo kila kitu huonekana kwenda tofauti? Kuanzia dakika ya kwanza unatoka kitandani? Ninaamini kwamba wote tulishawahi kuwa na nyakati kama hizo.

Ahadi kutoka kwa Mungu

Kwenye siku hizo, Mungu anatupa fursa zaidi kuishinda dhambi. Ambapo kila kitu huonekana kwenda tofauti, haioneshi kuhisi kama anatujali sana!

Lakini maneno ya Mungu yako wazi. “Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; nina Mungu mwaminifu ; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita muwezavyo; pamoja na lile jaribu atafanya na mlango  wakutokea, ili muweze kustahimili” 1 Wakotintho 10:13

Hiyo ina maana hata katika siku ambazo kila kitu huonekana kuwa kinyume nasi, inawezekana usiwe na chuki na hasira au kuanguka tunapojaribiwa.

Mfano wa Daudi: Mshindi asiye na woga

Ninakumbuka nyakati fulani nilipokuwa na moja ya siku hizi; ilionekana kama kila kitu kilikuwa kinyume na mimi. Nilipokuwa napanda kitandani jioni hiyo na nikifikiri kuhusu vitu vyote ambavyo vimetokea, Nilikumbushwa kwenye habari ya Daudi na Goliati kwenye agano la kale.

Daudi alikuwa ni kijana mdogo dhidi ya mtu aliyekuwa na umbile kubwa, lakini alikuwa amejaa roho wa Imani na aliamini katika Mungu hakika, kwamba hakuwa na woga. Katika roho hii ya Imani na nguvu aliweza kushinda na kumuua mtu mwenye umbile kubwa,na mwisho jeshi lote lilishindwa. Kwa sababu ya hili, wana wa Israeli wakapata amani tena, Ambapo mwanzo walikuwa wakisumbuliwa na wafilisti.

Maisha ya kushinda

Lakini nilijua kwamba ikiwa nilifanya hivi, kisha “maadui” wangu wangeweza kushinda. Kisha nisingeweza kuwashinda; wangeweza kunishinda. Badala ya kuitikia katika namna hii ningeweza kukataa kukubali kwenye vitu kama uchungu, chuki, au hasira. Kila muda nilipokuwa ninajaribiwa kwenye vitu hivi, ningeweza kusema “Hapana!” na kuomba msaada kuvishinda.

Mwisho wa siku, ningeweza kusema kwamba nilipigana kweli vita vigumu dhidi ya dhambi katika asili yangu-dhidi ya chuki na hasira na kutokuwa na Fadhili. Sikuwahi kukubali na kuhisi amani na furaha kujua kwamba Mungu kweli alinipa njia nje katika hali kama hizi. Nilishinda.

Na Mungu anataka iwe vivyo hivyo kwa hali zako! Wewe pia unaweza kushinda dhambi unayojaribiwa kupata amani ndandi yako, hata kwa nyakati hizi huonekana kama kila kitu kinaenda kinyume.

Chapisho hili linapatikana katika

Makala hii imejikita katika Makala ya Heather Crawford awali ilichapishwa https://activechristianity.org/  na ilibadilishwa kwa ruhusa kutumika kwenye tovuti hii.