Mkristo wa Jumatatu asubuhi ni nani?

Mkristo wa Jumatatu asubuhi ni nani?

Je, kile unachofanya kama Mkristo siku ya Jumatatu si swali muhimu zaidi?

22/4/20133 dk

Na Ukristo wa Utendaji

Mkristo wa Jumatatu asubuhi ni nani?

4 dak

Siku za mwisho wa wiki, kuna njia nyingi tofauti ambazo Wakristo huabudu na kupata uzoefu wa imani yao. Wengine wanaenda kwenye ibada ambazo zimejaa ibada za maombi, nyimbo na muziki, wengine wanaenda kwenye ibada ambapo kuna maombi ya uponyaji wa wagonjwa au mahubiri ya kutia moyo n.k. Lakini imani yetu ya kikristo ina maana gani katika maisha yetu ya kila siku. Jumatatu - na kwa wiki nzima?

Mitume wanasema nini kuhusu jinsi maisha ya Mkristo yanapaswa kuwa?

Inafaa kusoma jinsi mitume Paulo, Petro, Yakobo, na Yohana walivyoandika kuhusu maisha ya kila siku ya Mkristo katika kila aina ya hali - kila siku ya juma. Ilikuwa mioyoni mwao kwamba imani yetu ya Kikristo inapaswa kuongoza matendo yetu yote, maneno, na mawazo yetu.

Petro na Paulo waliona kuwa ni jambo la maana sana kwamba waume, wake, na watoto katika familia wanapaswa kutendeana kwa upendo na heshima, na pia kwamba tunapaswa kuwa wenye kutegemeka, wanyoofu na waadilifu katika sehemu zetu za kazi.

Paulo na Yakobo walisema kwamba imani yetu ya Kikristo inapaswa kutusaidia kutumia ulimi wetu kwa njia nzuri. Yakobo anaiandika kwa njia rahisi sana anaposema, “Mtu akidhani ya kuwa anayo dini, wala hauzuii ulimi wake kwa hatamu, hali akijidanganya moyo wake, dini yake mtu huyo haifai.” Yakobo 1:26.

Maisha ya Kikristo: Kuishi kulingana na amri za Mungu

Yohana anaandika mara kadhaa kwamba haitoshi tu kusema kitu, lakini kwamba kuishi kulingana nayo katika maisha ya kila siku ni muhimu zaidi. “Yeye asemaye, “Nimemjua, wala hazishiki amri zake, ni mwongo, wala kweli haimo ndani yake. Lakini yeye alishikaye neno lake, katika huyo upendo wa Mungu umekamilika kweli kweli. Katika hili twajua ya kuwa tumo ndani yake.” 1 Yohana 2:4-5. "Watoto wadogo, tusipende kwa neno wala kwa ulimi, bali kwa tendo na kweli." 1 Yohana 3:18.

Kuna hali nyingi ambazo tunaweza kuwa na wasiwasi. Paulo na Petro walijua jambo hilo vizuri sana, na Petro aandika hivi: “Huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulusha sana kwa mambo yenu.” 1 Petro 5:7.

Je, tunakuwaje tunapokwama kwenye foleni barabarani? Tunatumiaje pesa zetu? Tunatumiaje macho yetu - je, tunaruhusu macho yetu kutazama kila kitu, kwa mfano kwenye mtandao? Hebu tujiulize: imani hii ya Kikristo ambayo tunaisikia katika ibada za Kikristo siku za mwisho wa wiki - je, kweli inaongoza matendo yetu yote, maneno, na mawazo yetu siku saba kwa juma? Ni hapo tu ndipo ibada yetu itakapompendeza Mungu.

Chapisho hili linapatikana katika

Makala haya yanatokana na makala ya Jan-Hein Staal yaliyochapishwa awali kwenye https://activechristianity.org/ na yamebadilishwa kwa ruhusa ya matumizi kwenye tovuti hii.