Ulikuwaje mwaka mmoja uliopita ikilinganishwa na leo? Je, una uvumilivu na fadhili zaidi? Je, wewe ni mkarimu zaidi? Je, umekuwa bora katika kuonyesha kujali kweli kwa wengine?
Ikiwa sivyo, basi kwa nini?
Fikiria juu ya hili: Inamaanisha nini kuwa Mkristo mwenye bidii? Je, inamaanisha tu kwamba unasoma Biblia yako, kuomba kila siku na kwenda kanisani siku za Jumapili? Je, unafanya haya kwa sababu ndio jambo linalotakiwa kwa Mkristo, au kweli unaendelea mbele katika maisha yako?
Shiriki katika asili ya Mungu
Lengo letu kama Mkristo ni nini? Tunaweza kusoma hilo katika 2 Petro 1: 3-4: " Kwa kuwa uweza wake wa Uungu umetukirimia vitu vyote vipasavyo uzima na utauwa, kwa kumjua yeye aliyetuita kwa utukufu wake na wema wake mwenyewe. Tena kwa hayo ametukirimia ahadi kubwa mno, za thamani, ili kwamba kwa hizo mpate kuwa washirika wa tabia ya Uungu, mkiokolewa na uharibifu uliomo duniani kwa sababu ya tamaa.." Ni kauli ya ajabu kweli! Petro kwa kweli anasema kwamba hili ndilo lengo letu: kushiriki katika asili ya kimungu kupitia hali zetu hapa duniani! Hii ina maana kwamba mabadiliko makubwa yanapaswa kutokea ndani yetu.
Basi unachofanya ni nini ikiwa unahisi kuwa haujabadilika leo ukilinganisha na mwaka uliopita??
Swali ni: Je, unaona kwamba unahitaji kubadilika? Je, unategemea kabisa msaada wa Mungu kukuongoza katika siku yako? Je, unaona kwamba njia za Mungu ni kamilifu na wewe ni mwanadamu asiye mkamilifu, aliyejaa tabia ya kutenda dhambi? Au haufikiri unahitaji kubadilika? Umeridhika jinsi ulivyo?
"Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi." Ufunuo 3:17.
Kuwa makini daima
Kujitosheleza katika maisha yetu ya Kikristo ni hatari kubwa sana. Hatupaswi kamwe kusahau kwamba kwa asili sisi ni wanyonge, wenye huzuni, maskini, vipofu na uchi.
Maadamu wewe ni mnyenyekevukuto sha kuomba msaada, Roho Mtakatifu atakuongoza. Kitu kibaya zaidi ni kujiridhisha mwenyewe, - kufikiria hakuna chochote unachohitaji kufanyia kazi katika maisha yako. Mwishoni mwa Waebrania 11: 6 tunaweza kusoma: "... huwapa thawabu wale wamtafutao." Kutafuta kitu kwa bidii kunamaanisha kukifanya kwa umakini, na kufanya kila wakati. Kutafuta kwa bidii. Mungu anaweza kuongoza meli inayosogea, lakini si ile iliyosimama tu..
Ikiwa mtu atakuuliza leo ni nini unachokifanyia kazi katika maisha yako ya kikristo hivi sasa, je, utakuwa na jibu kwake?”? Ikiwa huna, basi una vipaumbele vingine katika maisha yako. Mambo mengine ambayo ni muhimu zaidi kwako kuliko maisha na Kristo, maisha ambayo unapata asili zaidi na zaidi ya Yesu. Umeridhika na kile ulicho nacho na haujisikii haja ya kuja mbali zaidi. Mithali 1:32 inasema: " Maana kurudi nyuma kwao wajinga kutawaua, Na kufanikiwa kwao wapumbavu kutawaangamiza."
Labda una maarifa na ulikuwa na vita vya kiroho maishani mwako, lakini hiyo inatosha? Je, umemaliza? La! Unahitaji kukua kila siku. Unapoenda kulala mwisho wa siku unaweza kufikiria nyuma na kufikiria juu ya chaguzi ulizofanya, ukiangalia kuwa umetumia fursa kukua. Je, hii si bora zaidi kuliko kuridhika? Je, si ni bora zaidi kuliko kutochukulia kwa uzito pale unapokuwa umejikwaa katika dhambi?
Kuona ukuu wa wito wetu
Tumeitwa kuja kwatika asili ya kimungu, kuwa kama Yesu (Warumi 8:29). Unawezaje kuridhika wewe mwenyewe kwa urahisi? Ni kwa sababu huoni jinsi ilivyo vibaya kubadilika na kupata zaidi asili ya Yesu siku baada ya siku ukiwa hapa duniani. Hujitahidi kwa bidii na kutumia vyema fursa zako za kufanya mapenzi ya Mungu! Je, kuna hali ambapo unaweza kusema: "Ninashukuru vya kutosha, sihitaji kushukuru zaidi," au, "Nilikuwa mkarimu jana kwa hivyo sihitaji kuwa mkarimu tena leo"?
Kila siku ni zawadi unayopokea ili uweze kukaribia asili ya kimungu. Unapaswa kuwa na mtazamo wa akili kila wakati kwamba unataka kuacha mapenzi yako mwenyewe kufanya mapenzi ya Mungu kila siku, kila wakati, kila sekunde! Hapo ndipo utaona mabadiliko makubwa ndani yako mwaka hadi mwaka! Mabadiliko yanayokuandaa kwa ajili ya mbingu!