Mipaka iliyowekwa na Mungu: Kusudi lake na maisha yetu

Mipaka iliyowekwa na Mungu: Kusudi lake na maisha yetu

Mungu mwenyewe ndiye anayedhibiti mipaka ya maisha yetu kwa lengo la kutusogeza karibu naye.

4/5/20214 dk

Na Ukristo wa Utendaji

Mipaka iliyowekwa na Mungu: Kusudi lake na maisha yetu

Mungu anataka kutuvuta karibu naye

Sisi sote tuna mipaka katika maisha yetu. Mipaka ni hali zetu, mahali tunapoishi, afya zetu, fedha zetu, na kadhalika. Mipaka au hali hizi zinaweza kubadilika wakati wa maisha yetu. Wakati fulani tunaweza kuzibadilisha sisi wenyewe na wakati mwingine hali ambazo haziko nje ya uwezo wetu zinaweza kuzibadilisha. Tunaweza kupoteza sehemu kubwa ya maisha yetu kutamani mipaka yetu iwe tofauti - wakati kwa kweli ni muhimu zaidi jinsi tunavyoishi ndani yake.

Paulo alisema katika Matendo 17:26-27: “Kutoka kwa mtu mmoja aliumba mataifa yote katika dunia yote. Aliamua hapo awali ni lini watainuka na kuanguka, na akaamua mipaka yao. Kusudi lake lilikuwa kwamba mataifa yatafute Mungu na labda kuhisi njia yao kumwelekea na kumpata—ingawa yeye hayuko mbali na yeyote kati yetu.” Kwa hiyo mwishowe, ni Mungu ndiye anayedhibiti mipaka katika maisha yetu na lengo lake katika kufanya hivyo ni kutuvuta karibu naye.

Ayubu alijifunza nini wakati mipaka yake ilibadilika

Mipaka (hali) ya Ayubu ilibadilika sana wakati wa maisha yake. Kwa ruhusa ya Mungu, Shetani aliharibu mali zote za Ayubu na kuwaua watoto wake 10 kwa siku moja. (Ona Ayubu 1.) Kwa kushangaza, hili lilikuwa jibu la Ayubu: “Ayubu aliposikia haya, akainuka, akararua vazi lake, akanyoa kichwa chake ili kuonyesha jinsi alivyohuzunika. Kisha akainama chini ili kumwabudu Mungu. Alisema: ‘Nilikuwa uchi nilipozaliwa, na nitakuwa uchi nitakapokufa. Bwana alinipa vitu hivi, na amevichukua. Lihimidiwe jina la BWANA.’ Katika hayo yote Ayubu hakutenda dhambi wala kumlaumu Mungu.” Ayubu 1:20-22.

Kisha mipaka ya Ayubu ikawa midogo zaidi Mungu alipompa Shetani ruhusa ya kuugusa mwili wake: “Shetani . . . Ayubu 2:7.

Mke na marafiki wa Ayubu walikuwa na hakika kwamba Ayubu alikuwa amemchukiza Bwana, lakini Ayubu alielewa kujiweka karibu zaidi na Mungu katika wakati huu, ili kwamba baadaye angeweza kusema: “Nilisikia habari zako kutoka kwa wengine; sasa nimekuona kwa macho yangu. Ndiyo maana najichukia na kukaa hapa kwenye vumbi na majivu kuonyesha huzuni yangu.” Ayubu 42:5-6. Alitumia mabadiliko hayo katika mipaka yake ili kupata uhusiano wenye nguvu zaidi pamoja na Mungu.

Uhusiano wa kudumu na Mungu

Chaguo hili la kujiweka karibu zaidi na Mungu katika majaribu ya maisha, na katika mipaka iliyobadilishwa majaribu haya yanaweza kuleta, ni jambo ambalo mashujaa wa imani kama Nuhu, Ibrahimu, Musa n.k wamefanya katika vizazi vyote. (Ona Waebrania 11.) Walikubali kwa furaha mabadiliko haya ya mara kwa mara yasiyopendeza ili kwamba walipata uzoefu wa “…kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao kwa bidii.” Waebrania 11:6.

Pia Paulo aliandika jinsi alivyojifunza kukabili hali kama hizo maishani mwake: “Ninajua jinsi ya kuishi nikiwa maskini, na najua jinsi ya kuishi ninapokuwa na vitu vingi. Nimejifunza siri ya kuwa na furaha wakati wowote katika kila jambo linalotokea, ninapokuwa na chakula cha kutosha na ninapokuwa na njaa, ninapokuwa na zaidi ya ninachohitaji na ninapokuwa sina vya kutosha. Nayaweza mambo yote katika Kristo, kwa maana Yeye hunitia nguvu.” Wafilipi 4:12-13.

Tunapotazama mipaka na hali zetu kwa njia hii, tutaona yale ambayo Yesu alisema: “Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma.” Yohana 17:3. Maisha yanakuwa ya kuvutia tunapoishi maisha yetu pamoja na Mungu, ambaye anatumia kila kitu tunachopitia ili kutuleta katika uhusiano wenye kina zaidi Naye na Mwanawe, ambao hutuongoza kuwa zaidi kama Yesu. (Warumi 8:28-29.)

Hatutapoteza tena wakati kutumainia mabadiliko katika mambo ya kidunia ambayo hayawezi kamwe kuleta uradhi wa kweli, lakini afadhali tutapata maisha ya kimbingu ambayo pia yanamaanisha ushirika wa kweli na wengine ambao wana lengo hili sawa.

Chapisho hili linapatikana katika

: Makala haya yanatokana na makala ya Steve Lenk yaliyochapishwa awali kwenye https://activechristianity.org/ na yamebadilishwa kwa ruhusa ya matumizi kwenye tovuti hii.