Ukweli mbaya juu ya kudharau watu.

Ukweli mbaya juu ya kudharau watu.

Wakati Julia alipoona jinsi alivyojaa kiburi na majivuno, alijua kuwa kuna kitu angeweza kufanya juu yake.

7/9/20173 dk

Na Ukristo wa Utendaji

Ukweli mbaya juu ya kudharau watu.

4 dak

Ilikuwa siku ya kawaida. Nilikuwa nimekaa kwenye chumba kilichojaa watu, wakati ghafla, niligundua kitu ambacho kilinichukiza.

Nilikuwa kwenye kozi ya mafunzo ya wiki moja kwa kazi yangu. Kulikuwa na watu wengine 10 kwenye chumba hicho. Mmoja wao alikuwa mtu ambaye nilidhani hakuwa mwerevu kama mimi. Ukweli ulikuwa, hakuwa tu "mwenye mtindo wa kisasa". Kila kitu alichosema na kufanya kilinifanya nitake kutumbua macho yangu.

Wakati wiki iliendelea, kwa mshtuko wangu, niligundua kuwa nilimdharau mtu huyu. Ukweli mbaya ni kwamba nilijiona bora kumliko, au kuwa juu yake. Nilimdharau.

Njia ya kawaida ya kufikiria

Mawazo ya kawaida yangesema kwamba aina hizi za mawazo ni kawaida kabisa; kwamba tutakutana na watu maishani ambao hatupendi, au hawapatani nao, au ambao ni tofauti sana na sisi. Lakini kama mwanafunzi wa Yesu, sitaki kuishi maisha yangu kulingana na "njia ya kawaida kufikiria”. Ninataka kuishi kulingana na mapenzi ya Mungu na kufuata nyayo za Yesu, ambaye, "alipojikuta katika umbo la mwanadamu, alijinyenyekeza na kuwa mtiifu hadi kifo, hata kifo cha msalabani.” Wafilipi 2: 7-8.

Katika sura hiyo hiyo Paulo aliandika: "Msitende jambo lolote kwa nia ya kujitukuza wala kujivuna, bali kwa unyenyekevu kila mtu amhesabu mwingine bora kuliko nafsi yake." Wafilipi 2: 3.

Niligundua juma hilo jinsi nilivyojaa kiburi na majivuno. Ikawa karaha sana kwangu. Niliona kwamba nilikuwa mbali sana na kile ninachotaka kuwa: mpole na mnyenyekevu moyoni kama Yesu.

Lakini pia najua kwamba sio lazima nivunjishwe moyo na kile ninachokiona kwangu. Nina matumaini makubwa na uwezekano wa kuwa mtu mpya kabisa, aliyebadilishwa kabisa kutoka kwa jinsi nilivyo. Sio bora kidogo tu, sio mnyenyekevu kidogo tu, lakini mtu mpya kabisa! Ambapo ninaona kila mtu yuko juu kuniliko, bila ubaguzi.

Kuwa kiumbe kipya

Ninaweza kufanya hivyo kwa kukubali ukweli kuhusu nilivyo kiasili, kwa kujinyenyekeza na kuwa mtiifu kwa mapenzi ya Mungu. Basi ninaweza kupigana dhidi ya dhambi katika asili yangu kwa nguvu ambayo Mungu hunipa nikiiomba. Ninajua kwamba wale wanaoshinda dhambi maishani mwao wana ahadi kwamba wanaweza kushiriki katika asili ya uungu. (2 Petro 1: 4.)

Soma zaidi: Inamaanisha nini kupata ushindi juu ya dhambi?

Nimefurahi sana kuwa huru kutoka kwa dhambi mbaya na zenye kuumiza zilizo katika asili yangu. Ninashukuru sana kwamba Yesu aliniwezesha kuwa kiumbe kipya kabisa.

“Kwa hiyo, ikiwa mtu yumo ndani ya Kristo, ni kiumbe kipya; mambo ya zamani yamepita; tazama, mambo yote yamekuwa mapya.” 2 Wakorintho 5:17.

Chapisho hili linapatikana katika

Makala hii inategemea Makala ya Julia Albig iliyochapishwa hapo awali kwenye https://activechristianity.org/ na imebadilishwa na ruhusa ya matumizi kwenye wavuti hii.