Maisha mapya na yenye furaha - kwa njia ya msalaba!

Maisha mapya na yenye furaha - kwa njia ya msalaba!

"Haijalishi unaishi wapi au wewe ni nani, unaweza kuwa na furaha kabisa."

10/11/20147 dk

Na Ukristo wa Utendaji

Maisha mapya na yenye furaha - kwa njia ya msalaba!

"Haijalishi unaishi wapi au wewe ni nani, unaweza kuwa na furaha kabisa," anasema Nadya.

Nadya ni mtu mtulivu na mwenye pumziko ambaye hajionyeshi mwenyewe. Lakini kuna joto na upendo kutoka kwake, na ningependa kujua inatoka wapi.

Alikulia katika mji mdogo na alipata malezi mazuri ya utotoni mzuri na salama pamoja na wazazi wake na dada zake wawili. Nadya alifanya vizuri shuleni na alihusika katika shughuli nyingi tofauti.

Lakini alipokuwa kijana, Nadya alianza kusikia watu wakilalamika kuhusu tabia yake. Walikuwa wakisema kwamba alikuwa mtu mwenye hasira sana. Na ilikuwa kweli. Nyumbani, wakati wowote mama yake alipomwomba afanye jambo lolote, itikio lake la kwanza akiwa kijana lilikuwa, “Kwa nini nifanye hivyo?” Na shuleni, siku zote alitaka kuwa sahihi, na alikuwa akibishana mara kwa mara hadi apate kile alichotaka.

Nyakati za Jioni, mara nyingi alikuwa akimtembelea bibi  yake Mkristo. Nadya hakukulia katika  Ukristo, lakini alipenda kumsikiliza bibi yake akisimulia hadithi kutoka katika  Biblia.

"Ilikuwa kama kutazama ulimwengu mwingine - ulimwengu ambao ulikuwa tofauti kabisa na ulimwengu nilioshi na ambapo kila kitu kilitegemea mawazo ya kibinadamu.

Hadithi kuhusu Yusufu ilinivutia sana. Aliuzwa kama mtumwa Misri na kutupwa gerezani; lakini bado alipata nguvu kutoka kwa Mungu za kuwa na furaha na shukrani kutoka kwa Mungu .”

Hatua ya kugeuka

Nadya aliona kwamba kulikuwa na tofauti kubwa kati ya maisha ya mashujaa wa imani katika Biblia na maisha yake mwenyewe. Alipokuwa na umri wa miaka 15, alifikia hatua ya badiliko ambayo ingebadili maisha yake milele. Alikua hamwamini Mungu, lakini mstari mfupi na rahisi ambao  bibi yake alimsomea kutoka katika Biblia ulimfumbua macho ajue Mungu ni nani. Mstari huu ulikuwa 1 Yohana 4:12 (CEB), “Hakuna mtu aliyewahi kumwona Mungu…”

Ghafla alielewa kwamba hangeweza kutarajia kumwona Mungu kwa macho yake mwenyewe. Hakuna mtu aliyekuwa amemwona. Ilibidi tu uamini.

Kuanzia wakati huo na kuendelea, alitaka kujua mengi kadiri awezavyo kuhusu Neno la Mungu. Angesoma Biblia mchana na usiku. "Ilikuwa kama maji yaliyo hai," anasema. Alimwona " Nadya mzee "

Baada ya muda mfupi, alianza kumuona tena “Nadya mzee ” akiwa na tamaa zake za asili za dhambi na mazoea yake ya zamani.

Neno la Mungu lilimpa shauku kubwa ya kumaliza haya yote. Haikutosha kwake tu kutozungumza wakati alipohisi hasira yake ikipanda. Alitaka kuwa huru; huru kutoka katika  ubinafsi; alimaliza na madai yake yote na kutoridhika ndani yake.

Alipobatizwa akiwa na umri wa miaka 16, Mchungaji huyo alimuuliza kwa nini alikuwa Mkristo. Alimwambia kwamba ushuhuda wake ulikuwa mstari katika Yohana 14:15, “Mkinipenda, mtazishika amri zangu.” Alimpenda Yesu na alitaka kushika amri zake, ambazo alikuwa amesoma sana kuzihusu.

“Baada ya kubatizwa, nilivunjika moyo sana. Tabia yangu ya zamani ya hasira ilianza kunisumbua zaidi. Nilikuwa Mkristo sasa, lakini bado sikuweza kubadilika. Nilihitaji msaada.”

 

Tumaini jipya

Nadya alisikia mara nyingi kwamba Yesu alikufa msalabani kwa ajili ya ondoleo la dhambi. Lakini hii haikumletea faraja tena.

Muda mfupi baadaye, baadhi ya Wakristo kutoka Brunstad Christian Church walitembelea kanisa lake. Aliwasikia wakiimba wimbo kutoka katika kitabu cha nyimbo walichokuja nacho, Wimbo ambao ulimpa tumaini jipya.

“Miongoni mwa mambo mengine, nilisikia wimbo wenye maneno, ‘Kwa watumwa wa dhambi nitaharakisha, Kwa maana usiku unakaribia.’ (*“Njia za Bwana” #347) ‘Hili ndilo ninalohitaji, ’ Nilifikiri.”

Hadi siku hiyo alijisikia kama "mtumwa" wa dhambi, kama mtumwa wa hasira yake, lakini sasa aliona msalaba kama njia ya kutoka kwa hasira yake - njia ya kuwa huru kutokana na hasira hii. Ingawa Yesu alikuwa hana hatia kabisa, alikufa msalabani pale Kalvari ili aweze kusamehe dhambi zetu.

“Lakini pia niliona kuwa msalaba ulikuwa zaidi ya huo. Yesu alisema Hapana kwa mapenzi yake kila siku, katika majaribu yote aliyokutana nayo. Alichagua kufanya mapenzi ya Mungu daima badala ya mapenzi yake mwenyewe. Katika Luka 9:23 Anatoa huu wito wa‘kujitwika msalaba wake kila siku’ - muda mrefu kabla ya kusulubishwa Kalvari.

Sasa alielewa kwamba Yesu hakusema tu Hapana kwa dhambi za nje ambazo Alijaribiwa kuzitenda kama vile maneno ya hasira, matendo mabaya, n.k. - Alipigana vita dhidi ya tamaa zote za ndani za dhambi zilizoishi katika asili Yake ya kibinadamu – Ubinafsi Wake— mapenzi, au “dhambi katika mwili”, kama Biblia inavyoiita katika Warumi 8:3.

Juu ya "msalaba huu wa kila siku" dhambi " iliuawa" kabla ya kuwa tamko au tendo. Yesu sio tu alikufa msalabani ili kutupa msamaha wa dhambi zetu, pia alitupa mfano ambao tunapaswa kufuata. Ukweli kwamba Yeye hakukubali kamwe alipojaribiwa kuwa na hasira, wivu, kuudhika, n.k., ulimpa Nadya uwezekano wa kufanya vivyo hivyo.

“Maneno ya Paul katika Wagalatia 2:20 yalipata maana mpya kabisa kwangu,” anasema. “Nimesulubiwa pamoja na Kristo; si mimi tena ninayeishi, bali Kristo yu hai ndani yangu.”

 

Alipata uzoefu kwamba msalaba unafanya kazi

Mambo yalianza kubadilika katika maisha yake. Anatabasamu anapofikiria jinsi mama yake alivyoshangaa alipomwomba binti yake mwenye umri wa miaka 17 amsaidie jambo fulani, naye akapata jibu, “Hakika, ninaweza kufanya hivyo,” hata kabla mama yake hajamaliza kuuliza swali hilo.

“Niligundua  kwamba  msalaba hunafanya kazi. Nilifikiria  kwamba ikiwa unafanya kazi katika mambo madogo, basi pia utafanya kazi   nitakapokutana na mambo makubwa zaidi, "anasema akiwa na tabasamu pana.

Matumaini na imani kwa siku zijazo

Ilikuwa faraja kubwa sana  hatimaye  kwamba anaweza kushinda. Hio ilimpa tumaini na imani kwa ajili ya siku zijazo - imani katika maisha ambayo angeweza kubadilika zaidi na zaidi, siku  baada ya siku . Badala ya kuwa mtu mwenye hasira na uchungu, angeweza kuwa na furaha na shukrani. Alipoulizwa kama bado anahitaji msalaba, ali jibu kuwa yeye si mkamilifu.

"Ninauhitaji msalaba zaidi kuliko hapo awali. Ingawa nimeshinda mambo mengi, Mungu anaendelea kunionyesha maeneo mapya ninapohitaji msalaba, ambapo ninahitaji kushinda. Kisha lazima niendelee kusema Hapana kwa mapenzi yangu binafsi, ili matunda ya Roho kama wema, wema n.k. yaweze kukua zaidi na zaidi katika maisha yangu."

Anatumia mstari katika Warumi 14:17 (NLT) kama mwongozo katika maisha yake, “Maana ufalme wa Mungu si kula wala kunywa, bali ni haki na amani na furaha katika Roho Mtakatifu.” Anapokuwa na amani na shangwe hiyo moyoni mwake, anajua kwamba anafuata mapenzi ya Mungu.

Anza katika hali ndogo

Alipoulizwa kama ana ushauri wowote kwa wasomaji ambao bado hawana imani katika maisha haya, anasema, "Mtumaini Mungu - siyo jinsi unavyoelewa mambo mwenyewe. Mungu ni muweza wa yote. Anaweza kubadilisha kila kitu. Anaweza kumfurahisha mtu asiye na furaha. Haijalishi unaishi wapi au wewe ni nani, unaweza kuwa na furaha sana.”

Ni jambo ambalo amepitia.

“Kwanza, mgeukie Mungu. Unahitaji kuwa tayari kumtumikia Mungu kwa moyo wako wote. Anza na vitu vidogo sana. Unapofanya hivyo, utaona kwamba Mungu ni mwaminifu. Yeye hufanya hivyo ili uweze kuwa na furaha na shukrani siku zote, iwe hisia zako ziende juu au chini na hata hali yako iweje.”

Makala haya yanatokana na makala ya I.M. Larsen yaliyochapishwa awali kwenye https://activechristianity.org/ na yamebadilishwa kwa ruhusa ya matumizi kwenye tovuti hii.

Shiriki