Siku hii ndiyo aliyoifanya Bwana!

Siku hii ndiyo aliyoifanya Bwana!

: Kila siku ni tajiri na zawadi ya thamani kutoka kwa Mungu, na neema mpya na fursa mpya.

23/9/20153 dk

Na Ukristo wa Utendaji

Siku hii ndiyo aliyoifanya Bwana!

4 dak

“Siku hii ndiyo aliyoifanya BWANA, tutashangilia na kufurahia” Zaburi 118:24. Kila siku ni yenye utajiri na zawadi ya thamani kutoka kwa Mungu, na neema mpya na fursa mpya.

Yesu anasema kwamba hii siku moja pekee, na hatupaswi kuwa na hofu juu ya kesho. Hata kama imeenda vibaya hapo kabla, inawezikana ikawa siku mpya na yenye utukufu. Kama kuna jambo ambalo linasumbua dhamira zetu kutokana na yaliyopita, tuna neema ya kutosha Zaidi na nguvu kuyaweka sawa leo.

Tufurahi

Kama Biblia inavyosema, tufurahi kwa kila siku. Ni Bwana ndiye aliyeifanya na kuipanga kwa ajili yetu. Ni mwaminifu na hujali ili leo tusijaribiwe na kupimwa zaidi ya tunavyoweza kustahimili. Atatengeneza jaribu na kufanya njia ya kustahimili. (1Wakorintho 10:13) Na tunatambua kwamba mambo yote yatafanyika pamoja kwa mazuri yetu. (Warumi 8:28) Leo Mungu amepanga kila mambo yote mema tunayopaswa kufanya, na tutakua na neema ya kutosha na nguvu kuyafanya. (Waefeso 2:10)

Tunapaswa kujifunza kuishi kana kwamba kila siku ni siku yetu ya mwisho.

Leo inapaswa kuwa siku pekee, siku ya mwisho ambayo tunapaswa kuonesha wema wote na upendo kwa kila mmoja. Leo tunapaswa kulifanya jina la Yesu kuwa kuu katika kila jambo tunenalo na kutenda na kuwa wema kwa watu wote, hata kwa wale ambao si wakarimu kwetu.

Ni leo tutavumilia, tutateseka, na tutabeba mambo yote kwa furaha, kwa kuamini kabisa kwamba Mungu yupo katika udhibiti. Leo tutakuwa jasiri na kutopoteza ujasiri, lakini badala yake tutatazamia vitu visivyoonekana, kwa sababu shida zetu zitakuwa nyepesi, zitadumu kwa muda mfupi tu na zitatupa utukufu wa milele ambao ni mkuu kuliko shida. (2Wakorintho 4:16-18)

Hii ndiyo siku aliyoifanya bwana

“Kwa maana maagizo haya nikuagizayo leo, si mazito mno kwako, wala si mbali.” Kumbukumbu la Torati 30:11. “Lakini neno li karibu nawe sana, li katika kinywa chako na moyo wako, upate kulifanya. Angalia namechecked leo mbele yako uzima na mema, na mauti na mabaya; Kwa hivi nikuagizavyo leo kumpenda BWANA, Mungu wako, kuenenda katika njia zake, na kushika maagizo yake, na amri zake, na hukumu zake, upate kuwa hai na kuongezeka; BWANA, Mungu wako, apate kukubariki katika nchi uingiayo kuimiliki.” Kumbukumbu la Torati 30:14-16.

Leo nachagua kati ya uzima na mafanikio, ama kifo na madhara ya kupokea ama kukataa sheria za Mungu zilizoandikwa moyoni mwangu. “Kwa hiyo, kama anenavyo roho mtakatifu, Leo, kama matasikia sauti yake, msifanye migumu mioyo yenu…..” Waebrania 3:7-8.

Uamzi tunaofanya leo ni muhimu katika maisha yetu ya milele! Yesu atakuja kuwachukua wanaomsubiri leo na walio tayari kukutana nae. Ni wana wa nuru na mchana.

Siku hii ndiyo aliyoifanya BWANA!

Chapisho hili linapatikana katika

Makala hii imejikita kwenye Makala ya Aksel J. Smith, awali ilichapishwa ikiwa na kichwa cha Habari “Hii ni siku” kwenye jarida la BCC “Skjulte Skatter” (“Hazina zilizojificha”) Mwaka 1975. Imechukuliwa na kupewa ruhusa kutumika kwenye tovuti hii.