Je, inawezekana kuwa huru kutoka katika dhambi?

Je, inawezekana kuwa huru kutoka katika dhambi?

Inaweza kuwa vigumu kwa wengi kuamini, lakini inawezekana kabisa kuwa huru kutoka katika dhambi.

30/3/20154 dk

Na Ukristo wa Utendaji

Je, inawezekana kuwa huru kutoka katika dhambi?

6 dak

Ingawa inaweza kuwa vigumu kwa wengi kuamini, Biblia inatuambia wazi kwamba katika Agano Jipya inawezekana kabisa kuwa huru kutoka katika dhambi—sio tu matendo ya dhambi yanayoonekana, ya nje, lakini pia mzizi wa dhambi ambao nimerithi na ambao huishi katika asili yangu ya kibinadamu.

Asili yetu ya kibinadamu

Kwa asili, sisi daima tunataka kufanya mapenzi yetu wenyewe, ambayo kwa maneno mengine ni dhambi. Mimi mwenyewe siwezi kushinda tabia hizi, dhambi hii ambayo inaishi katika asili yangu ya kibinadamu.

Tunaweza kuona hili katika mifano tuliyo nayo katika Agano la Kale. Kila mwaka kuhani mkuu alilazimika kuingia mahali Patakatifu na damu ya mbuzi au ng'ombe ili kupata msamaha kwa dhambi zake mwenyewe na dhambi za watu. Hata wale waliomcha Mungu zaidi, wale ambao hawakuwa na hatia kwa nje kulingana na sheria, hawakuweza kudhibiti dhambi iliyoishi ndani yao, na dhambi hizi zingerudi tena na tena.

Dhabihu ya Yesu

Kwa kumtoa mnyama katika Agano la Kale, watu wangeweza kupokea msamaha kwa dhambi walizofanya, lakini damu ya wanyama haikuweza kuondoa tamaa za dhambi ambazo ziliishi katika asili yao ya kibinadamu, kwa kuwa dhabihu nyingine ilihitajika. Dhabihu hii ililetwa na Yesu.

Tunaweza kusoma juu ya hili katika Waebrania 10: 4-7: "Maana haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi. Kwa hiyo ajapo ulimwenguni, asema, Dhabihu na toleo hukutaka, lakini mwili uliniwekea tayari; sadaka za kuteketezwa na sadaka za dhambi ukupendezwa nazo; Ndipo niliposema, Tazama, nimekuja (katika gombo la chuo nimeandikiwa) niyafanye mapenzi yako, Mungu.

"Nimekuja kufanya mapenzi yako."Ilikuwa katika mwili wake kwamba Yesu alileta dhabihu hii, na dhabihu hii ilikuwa mapenzi yake mwenyewe, ambayo alijitoa kufanya mapenzi ya Mungu. Hakuwahi kuingia katika tamaa za dhambi na tamaa za asili yake ya kibinadamu (mwili wake) ambazo alirithi wakati alipozaliwa ulimwenguni, kwa hivyo Yeye kamwe hakutenda dhambi, ingawa alijaribiwa. (Waebrania 4:15.) Kwa njia hii alifanya iwezekane kwetu kufuata hatua Zake na kuwa na ushirika na Mungu, ikiwa sisi pia kama Yesu, katika nguvu ya Roho Mtakatifu kamwe hatukubali tunapojaribiwa. (1 Petro 2:21.)

"Basi ndugu, kwa kuwa tuna ujasiri wa kupaingia patakatifu kwa damu ya Yesu, njia ile aliyotuanzia iliyo mpya, iliyo hai, ipitayo katika pazia, yaani, mwili wake..."  Waebrania 10:19-20.

Damu ambayo Yesu alienda nayo mahali patakatifu, ambapo Mungu alikuwapo, ilikuwa "damu" ya mapenzi yake mwenyewe, na hii ilifanyika mara moja kwa wote. Tamaa za dhambi katika asili yake ya kibinadamu kwa kweli ziliuawa ndani yake, kwa hivyo hazikurudi tena kama ilivyokuwa katika Agano la Kale, na kwa hivyo hakukuwa na haja ya dhabihu za kila mwaka kupokea msamaha.

Lakini vipi kuhusu dhambi katika asili yetu?

Kwa sababu ya dhabihu ya Yesu, alipokea uwezo wa kusamehe dhambi ambazo tumefanya, ikiwa kweli tunataka kumfuata. Hii inafanya iwezekane kwetu kuanza upya, lakini pia tunaona kila siku kwamba dhambi tuliyo nayo katika asili yetu ya kibinadamu, haijaondolewa na msamaha.

Njia pekee ya kumaliza dhambi katika asili yangu ya kibinadamu, katika mwili wangu, ni kwenda kwa njia ile ile ambayo Yesu alienda. Imeandikwa kwamba Yeye ni mtangulizi wetu [GS1] [IH2]  (Waebrania 6:20), na alifanya hii "njia mpya na hai ... kwa njia ya mwili wake" ili tumfuate.

"Kwa sababu ndilo mliloitiwa; maana Kristo naye aliteswa kwa ajili yenu, akawaachia kielelezo, mfuuate nyayo zake. Yeye hakutenda dhambi, wala hila haikuonekana kinywani mwake." 1 Petro 2:21-22. Kufuata katika hatua Zake kunamaanisha kwamba sitendi dhambi pia, na hii inawezekana kupitia nguvu ya Roho Mtakatifu, kwa kusema Hapana mwenyewe na kuchukia tamaa za dhambi katika mwili wangu. Ndipo dhambi ambayo ninajaribiwa itauawa ndani yangu, ili dhambi isifanyike. Kwa hivyo niko huru kutoka kwa dhambi hiyo!

"Basi kwa kuwa Kriato aliteswa katika mwili wake, ninyi nanyi jivikeni silaha ya nia ileile; kwa maana yeye aliyeteswa katika mwili ameachana na dhambi. Tangu sasa msiendelee kuishi katika tamaa za wanadamu, bali katika mapenzi ya Mungu, wakati wenu uliobaki wakukaa hapa duniani.." 1 Petro 4:1-2.

"Basi, kama ni hivyo, ndugu, tu wadeni, si wa mwili tuishi kwa kufuata mambo ya mwili, kwa maana kama tukiishi kwa kufuata mambo ya mwili, mwataka kufa; bali kama mkiyafisha matendo ya mwili kwa roho, mtaishi." Warumi 8:12-13.


 [GS1]Unganisha na kifungu cha 36b - Yesu: Mtangulizi, Mtangulizi

 [IH2]Unganisha kwenye makala:

https://activechristianity.africa/jesus-pioneer-forerunner

Chapisho hili linapatikana katika

Makala hii ilichapishwa awali kwenye https://activechristianity.org/ na imebadilishwa na ruhusa ya matumizi kwenye tovuti hii.